TAARIFA KWA UMMA
IMETOLEWA LEO 02/02/2016
BAKWATA MKOA DAR HAINA MAMLAKA YA KUITAKA CUF KUINGIA KWENYE UCHAGUZI
ALHAD MUSSA ANASHUGHULISHWA ZAIDI NA DUNIA KULIKO KUSIMAMIA HAKI
NI VYEMA AKAJIFUNZA KWA VIONGOZI WA KIKRISTO KUHUSU ZANZIBAR
CUF - Chama cha Wananchi, tunasikisitishwa na kushangazwa na kauli ilitolewa leo na Alhad Mussa, kuunga Mkono ukiukwaji wa Demokrasia uliofanywa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) sio tu Kuna onyesha sura halisi ya Kiongozi huyo wa Kiroho Lakini pia kinamuonyesha jinsi asivyokua na khofu ya Kukabiliana na Mola wake kwa Matendo atendayo hapa Duniani au kwa kauli atowazo kama Kiongozi wa Dini. Cuf tumezoea kumsikia mara kadhaa akiwashauli Viongozi wa Kisiasa na Viongozi wenziwe wa Kiroho kwamba wasichanganye Dini na Siasa, Lakini leo ajabu kwetu kumuona Alhad Mussa sio tu akichanganya Lakini akichupa Mipaka na kuitaka Cuf ishiriki kwenye Uchaguzi. Bila Shaka Alhad Mussa ni Mwanachama wa CCM kama ambavyo aliwahi kujitambulisha kwenye moja ya Shughuli za Kiserikali zilizopambwa na kunogeshwa na Viongozi wa Chama cha Mapinduzi. Kwakua umeshindwa kusimamia Maendeleo ya Jamii unayoiongoza, tunahakika Huku unapokuja Sasa hutapaweza. Hali ya Zanzibar kwa Sasa ni tete na si suala jepesi kama Vile kwenda Ofisi za Bakwata pale Kinondoni. CUF tunaipuza kauli yako kama tunavyopuuza Uchafu wowote ule utakao kwenye Majumba yetu. CUF inawapongeza Viongozi wa Dini ya Kikristo ambao wameshatoa kauli ya Kupinga Ubakwaji wa Demokrasia na Maamuzi ya Wazanzibar. Tuna mtaka Alhad Mussa ajifunze kupitia kwa Viongozi Hao wa Dini ya Kikristo ambao wameonyesha uadilifu Mkubwa kwa kukemea ubabaishaji unaofanywa na ZEC. Kama Hana cha kujifunza kutoka kwa Viongozi wenziwe wa Kiroho kama alivyo yeye, basi ajifunze kwa Makada wa CCM ambao wanaijua vizuri CCM zaidi yake, ambao ni Benard Membe, Joseph Butiku na Dr Salim Ahmed Salim. Hata hivyo katika ile dhana au ile nia ya Kushughulishwa zaidi na Dunia kuliko kazi ya kulingania Waumini wake kutenda Mema na kuhimiza Maendeleo yao, Kielimu, Kiafya na Kiuchumi, Bila Shaka atakua amefikia Lengo la kuwafurahisha Maswahiba zake. CUF - Chama cha Wananchi hakiingii kwenye Uchaguzi hata iweje.
Huo ndio Msimamo wa Baraza Kuu la Uongozi Taifa.
Taarifa zinazowiana
- CUF Wanawake wawapa 'take-care' Mutungi, Lipumba
- NDUNGAI NI NYOKA ANETAFUNA MKIANI
- MAHAKAMA YAIPIGA NA CHINI HOJA ZA SERIKALI DHIDI YA KESI YA CUF
- MAAAMUZI YA BARAZA KUU LA UONGOZI LA TAIFA LA THE CIVIC UNITED FRONT (CUF - CHAMA CHA WANANCHI) KUHUSIANA NA HUJUMA ZA DOLA DHIDI YA CUF
- Mbunge wa Temeke akamatwa kihuni
- SITAKI KUMUONA LIPUMBA ASEMA MBUNGE WA TEMEKE
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
- How Magufuli will solve Tanzania political crisis
- Ziara ya Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Kisiwani Pemba February 2017
- MAZOMBIE NI POLISI SHIRIKISHI
- Mkutano wa CUF na viongozi wa ngazi za Wilaya na Majimbo ya UngujaCUF na viongozi wa ngazi za Wilaya na Majimbo ya Unguja
- JAJI FRANCIS MUTUNGI NDIYE CHANZO CHA VURUGU ZINAZOENDELEA NDANI YA CUF HANA USAFI WA MAADILI (MORAL AUTHORITY AND MORAL EXCELLENCE) ASIWADANGANYE WATANZANIA:
- Wamasai wapewa Vitambulisho Zanzibar
No comments:
Post a Comment