TAARIFA RASMI:
Kundi la WAHUNI lililotumwa kuvamia Mkutano Mkuu wa CUF na kuuvuruga limeendelea na vikao vyake jana na leo na limefikia maazimio kuwa litavamia OFISI KUU ya CUF Buguruni ili kumrejeshea Lipumba Uenyekiti kwa kumleta ofisini kwa nguvu.
Kesho kundi hilo litakuwa nyumbani kwa Prof. Lipumba ili kukubaliana naye juu ya mpango wa namna ya kutekeleza azma hiyo. Na kwa namna ambavyo Prof. amekuwa hatabiriki huenda akakubali mpango huo kama alivyokubali kuletwa na kuvamia na kuvuruga mkutano mkuu maalum wa CUF.
Hakika, kama Lipumba atakubali kutekeleza kitendo hicho atakuwa ni Profesa wa ajabu kupata kutokea hapa duniani. Namuombea sana Lipumba ambaye ni "Alhaji" aanze kujitambua na nafsi yake imsute kwamba haya anayoyapanga na kuyatekeleza yanaidhalilisha sana familia yake, wasomi wenzake, wanasiasa wenzake na kuvunja kabisa heshima kubwa ambayo aliijenga kwa miaka 20.
Kila mmoja wetu umuombee Lipumba.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
- TAARIFA KWA UMMA
- MAALIM SEIF ACHUKUA FOMU YA URAIS
- Ziara ya Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif Kisiwani Pemba February 2017
- Katibu Mkuu akutana na Mchungaji Gwajima
- Mkutano wa CUF na viongozi wa ngazi za Wilaya na Majimbo ya UngujaCUF na viongozi wa ngazi za Wilaya na Majimbo ya Unguja
- CUF Wanawake wawapa 'take-care' Mutungi, Lipumba
- Lowassa aiteka ngome ya Magufuli Chato
No comments:
Post a Comment