TAARIFA RASMI:
Kundi la WAHUNI lililotumwa kuvamia Mkutano Mkuu wa CUF na kuuvuruga limeendelea na vikao vyake jana na leo na limefikia maazimio kuwa litavamia OFISI KUU ya CUF Buguruni ili kumrejeshea Lipumba Uenyekiti kwa kumleta ofisini kwa nguvu.
Kesho kundi hilo litakuwa nyumbani kwa Prof. Lipumba ili kukubaliana naye juu ya mpango wa namna ya kutekeleza azma hiyo. Na kwa namna ambavyo Prof. amekuwa hatabiriki huenda akakubali mpango huo kama alivyokubali kuletwa na kuvamia na kuvuruga mkutano mkuu maalum wa CUF.
Hakika, kama Lipumba atakubali kutekeleza kitendo hicho atakuwa ni Profesa wa ajabu kupata kutokea hapa duniani. Namuombea sana Lipumba ambaye ni "Alhaji" aanze kujitambua na nafsi yake imsute kwamba haya anayoyapanga na kuyatekeleza yanaidhalilisha sana familia yake, wasomi wenzake, wanasiasa wenzake na kuvunja kabisa heshima kubwa ambayo aliijenga kwa miaka 20.
Kila mmoja wetu umuombee Lipumba.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Popular Posts
- KIKWETE NDIO ALIEVURUGA DEMOKRASIA YA ZANZIBAR
- HOTUBA YA KIONGOZI WA UPINZANI BUNGENI (KUB) MHESHIMIWA FREEMAN AIKAELI MBOWE (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAONI YA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KATIKA OFISI YA WAZIRI MKUU KWA MWAKA WA FEDHA 2016/17
- Kesi YA CUF DHIDI YA RITA KUUNGURUMA JULAI 10
- TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
- MBUNGE WA STONE TOWN ALI SALEH AWASOMESHA SHERIA BUNGENI
- Kwa la Zanzibar, Magufuli apewe nafasi kabla lawama
- MAALIM SEIF AWAPANDISHA RITA MAHAKAMANI
No comments:
Post a Comment