Headlines News :
KARIBU CUF DIASPORA NETWORK - CUF HAKI SAWA KWA WOTE...TEGEMEA KILA JIPYA NA ZURI KUTOKA KWETU...LIKE PAGE YETU KWENYE FACEBOOK

MAALIM SEIF ACHUKUA FOMU YA URAIS

 Maalim Seif Sharif Hamad leo alasiri amechukua fomu za kuomba kuteuliwa na CUF kuwa mgombea wake kwa nafasi ya Urais wa Zanzibar. Alichukua fomu hiyo katika Ofisi za Chama Wilaya ya Magharibi 'A' huko Bububu, nje kidogo ya Mji wa Zanzibar katika hafla ndogo iliyojaa shamra shamra huku akiwa amesindikizwa na mamia ya wapenzi wake. 

SAFARI IMEANZA: Maalim Seif Sharif Hamad leo alasiri amechukua fomu za kuomba kuteuliwa na CUF kuwa mgombea wake kwa nafasi ya Urais wa Zanzibar. Alichukua fomu hiyo katika Ofisi za Chama Wilaya ya Magharibi 'A' huko Bububu, nje kidogo ya Mji wa Zanzibar katika hafla ndogo iliyojaa shamra shamra huku akiwa amesindikizwa na mamia ya wapenzi wake.

Mamia ya wananchi wa Zanzibar leo walifika kushuhudia uchukuaji fomu wa Mgombea huyu wa Urais wa Zanzibar.

UONGOZI WA CHAMA CHA CUF

The Civic United Front (CUF- Chama cha Wananchi). CUF ni chama cha uliberali wa kidemokrasia ambacho kauli mbiu yake ni Haki Sawa kwa Wote. CUF inasimamia elimu bora, afya madhubuti, mfumo adilifu wa kodi, Muungano wa haki, siasa kuwa utumishi ulioutukuka kwa umma na fursa sawa katika kujiendeleza kiuchumi, kijamii na kisiasa.
Mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba
Mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba
HAKI SAWA KWA WOTE
Kaulimbiu ya Haki Sawa kwa Wote inalenga visheni ya CUF ya jamii tuitakayo. Hiyo ni jamii yenye wananchi wanaopendana, kuheshimiana, kuhurumiana, na wanaochukia uonevu, ukandamizaji na ubaguzi. Msingi Mkuu wa CUF ni haki za binaadamu na demokrasia na hivyo suala la usawa lina nafasi ya pekee katika kuijenga jamii inayokusudiwa na Chama chetu.
Azma ni kujenga jamii ambayo itahakikisha inapiga vita ubaguzi wa kila aina na ambayo itahakikisha kila mwananchi anathaminiwa utu wake, na ana haki na fursa sawa katika nyanja zote za maisha yake.
Lengo ni kujenga jamii ya demokrasia ya kweli na yenye kuongozwa na utawala wa sheria na Serikali nzuri (good governance), ambayo msingi wake ni kuwekwa madarakani na wananchi wenyewe.
Shabaha, Malengo na Madhumuni makuu ya CUF yameelezwa kwa urefu katika Katiba yake. Lakini kwa ufupi Shabaha kuu ya CUF ni kuona kwamba nchi yetu na wananchi wake wote wamepata uhuru wa kweli na kujigomboa na mapepe yaliyobaki baada ya ukoloni mkongwe kuondoka na, pia, kujikinga na athari za ukoloni mamboleo. CUF inakusudia kuhakikisha kwamba uwezo wa kuiongoza nchi na wa kutoa maamuzi mazito ya mambo makubwa ya Taifa uko mikononi mwa Watanzania wenyewe.
CUF siku zote itaongoza juhudi za wananchi zenye kuelekezwa katika kuiletea nchi yetu ukombozi wa kiuchumi. CUF itatilia maanani umuhimu wa rasilmali za nchi yetu kuwanufaisha wananchi wenyewe. Katika kufikia lengo hilo CUF itakuwa na uangalifu mkubwa katika kuwashirikisha wageni wenye uwezo wa fedha na teknolojia. Wimbo wa Taifa wa CUF unasema hivi:
Ni haki sawa kwa watu wote, kuendeleza taifa letuUtajirisho itikadi yetu, tukatae kuonewa.Siasa itumikie, uchumi wa Nchi yetuNi mwiko huo uchumi, kutumikia siasa
Wimbo huu unabeba mantiki nzima ya itikadi, falsafa na sera za CUF.
ITIKADI YA ULIBERALI
Makamu Mwenyekiti wa CUF, Juma Duni Haji
Makamu Mwenyekiti wa CUF, Juma Duni Haji
Itikadi kuu ya Chama cha Wananchi (CUF) ni Uliberali ambayo inalenga kuwazindua wananchi waweze kuitumia neema waliyopewa na Mwenyezi Mungu kwa manufaa yao binafsi na Taifa kwa ujumla. CUF inaamini kuwa Tanzania ni nchi tajiri kwa rasilimali na watu, lakini imefanywa kuwa masikini kwa kukoseshwa uongozi wenye sera na mtazamo (dira) wa kimaendeleo.
Inaposema Tanzania ina neema, CUF inakusudia uwezo wa akili na nguvu pamoja na utajiri wa asili tulinao. Nchi hii inao utajiri mkubwa wa ardhi ifaayo kwa kuzalisha mazao ya aina mbalimbali na inao utajiri mkubwa wa maji ya mito maziwa na bahari.
Itikadi ya Utajirisho inamhamasisha mwananchi ili aweze kuutumia ipasavyo utajiri wetu wa ardhi, bahari na madini ya thamani kama dhahabu, almasi, gesi, na tanzanite.
Kuhusu siasa, CUF kinasimama kama chama halisi na makini cha kisiasa kinachotumia siasa kwa maana yake halisi kufanya siasa kufikia malengo na dhamira yake kwa njia za kisiasa. CUF inasisitiza kuwa siasa si mchezo mchafu, ingawa inafahamu kwamba CCM imezifanya siasa zionekane hivyo kutokana na viongozi wake kuiharibu siasa kutokana na ulaghai wao kwa Watanzania. Kwa hivyo, mwelekeo wa siasa ya Chama Cha Wananchi ni kuwaelimisha na kuwaandaa wana-CUF na Watanzania wote katika kutoa utumishi wa kuridhisha kwa wananchi ili kurudisha hadhi na heshima ya siasa kama utumishi uliotukuka kwa umma.
Kuhusu mamlaka ya dola, CUF inaamini kwamba Serikali ndiyo dola na kwamba mamlaka yake yanapatikana kutokana na ridhaa ya wananchi kwa kufanyika uchaguzi ulio halali na huru na Serikali hiyo lazima iweajibike huko huko kwa wananchi. Kwa mujibu wa Itikadi hii, Serikali itakayoundwa na CUF lazima iwajibike kwa wananchi. Ndani ya Serikali ya CUF, kwa hivyo, hakutokuwa na nafasi ya walaghai wachache kuendesha mambo kwa ujanja, ufisadi na utapeli kama ambao umekuwa ukitekelezwa na viongozi wa serikali za CCM.
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad.
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad.
Kwenye uchumi na maendeleo, CUF inakusudia kujenga uchumi ulio imara kwa kuanzisha taratibu za kiuchumi zainazowashawishi kwa kadiri ya uwezo wao na kuchangia Taifa kwa ziada wapatayo. Mtazamo wa CUF kijumla ni wa kiliberali, kwa hivyo uhuru wa mtu binafsi kujiendeleza na kutumia fursa zilizopo kujinufaisha na kulinufaisha Taifa.
Kuhusu ardhi, CUF inachukulia kuwa ni mali ya watu wote, hivyo Serikali ya CUF itasimamia matumizi yake kwa uangalifu mkubwa. Ardhi itamilikiwa na wananchi wenyewe au Serikali yao. Kwa hivyo, ingawa CUF inakaribisha uwekezaji rasilimali kutoka nje, lakini Serikali yake haitomilikisha ardhi kwa wageni. Iwapo mwekezaji anahitaji ardhi kwa ujenzi wa kiwanda, kuendesha shughuli za kilimo au kuendeshea shughuli nyinginezo, mwekezaji huyo atawajibika kuingia ubia na mwananchi ambaye ndie atakayemilikishwa ardhi inayohitajika.
Kuhusu elimu, CUF imekusudia kutoa elimu ya darasa la kwanza hadi la kumi na mbili bure katika mashule yenye vifaa na walimu wenye sifa ya kufanya kazi hiyo wala sio katika hali ya sasa ambapo shule zilizopo hazina vifaa vya kutosha wala walimu wenye sifa hasa za kuwa walimu. CUF inaamini kwa elimu ndio msingi wa ujenzi wa taifa na kwamba taifa lisilo na watu walioelimika haliwezi kwenda mbele. Kusoma na kuelimika ni haki ya kila mwananchi na CUF inakusudia kuilinda na kuigawa haki hiyo kwa wenyewe, wananchi.
Kama ilivyo elimu, CUF inaamini kuwa afya nayo ni haki ya msingi ya kibinaadamu. Kwa hivyo, inakusudia kuboresha huduma za kinga pamoja na zile za tiba. Katika kulifanikisha hili, CUF itahakikisha kuwa mahospitali yaliyopo yanapatiwa vifaa bora pamoja na kuzingatia mafunzo kwa wafanyakazi.
Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Tanzania Bara), Magdalena Sakaya.
Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Tanzania Bara), Magdalena Sakaya.
Kwenye nyanja ya wafanyakazi, Serikali ya CUF inakusudia kupanga pato la mfanyakazi kwa saa wala sio kwa mwezi. Utaratibu huu ni wenye manufaa kwa pande zote mbili, wakati mfanyakazi anajitahidi kufanyakazi kwa masaa mengi ili ajipatie donge nono, mwajiri ananufaika kwa kulipa kulingana na kazi iliyofanywa.
Kuhusu umeme na maji, CUF inasisitiza kuwa kulingana na umuhimu wa huduma hizi kwa uhai na uchumi, Serikali yake itahakikisha kuwa wananchi wanapatiwa maji pale walipo na kunakuwepo umeme wa uhakika katika sehemu zote zilizokubalika kupata huduma hiyo.
Kwenye ushuru, Serikali ya CUF itahakikisha kwamba baadhi ya ushuru unaokusanywa na Serikali Kuu unahamishiwa Serikali za Mitaa na Serikali hizi zinakuwa bunifu.
Juu ya mabenki na huduma za fedha, Serikali ya CUF inakusudia kurekebisha mfumo wa uendeshaji wa Mabenki hapa nchini. Katika mabadiliko hayo, mabenki na taasisi nyingine za kifedha zitajiendesha kibiashara huku zikizingatia kutoa fursa ya kuwahudumia wananchi wote kwa kuondoa masharti yanayokwamisha wananchi wa kawaida kunufaika na huduma hiyo.
Kilimo kitapewa umuhimu mkubwa na wakulima wananchi watasaidiwa kuboresha njia zao za ukulima. Kwa sababu ardhi ndio rasilmali kuu ya nchi yetu basi ni wajibu wetu kuhakikisha kwamba ardhi yetu inatumika vyema.
Hivyo watumiaji wote wa ardhi watashawishiwa na kuelimishwa juu ya matumizi bora ya ardhi ili ardhi itoe mazao bora na mengi na wakati huo huo kuwahakikishia wakulima bei nzuri za mazao yao ili zilingane na juhudi zao na ubora wa mazao yao. Nia ni kuwafanya wananchi wawe na maisha mazuri kutokama na rasilmali ya nchi na juhudi zao.
Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Mhe. Nassor Mazrui.
Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Mhe. Nassor Mazrui.
Sekta za viwanda na madini zitapewa mwelekeo mpya ambao utakidhi hali halisi na ambao utatawaliwa na matumizi sahihi ya sayansi na teknolojia na sekta hizi zitaongozwa na wataalamu waliofunzwa na kufunzika, zitapata usimamizi wa makini na zitafanywa ziweze kuzalisha bidhaa zinazokidhi mahitaji ya masoko ya kimataifa ili bidhaa hizo ziweze kuuzika kwa urahisi.
Na kwenye suala la muhimu kwa uhai wa Taifa hili kama taifa, yaani Muungano, CUF inatambua umuhimu wa Muungano uliopo baina ya Tanganyika na Zanzibar bali inataka pawepo na Muungano wa ukweli unaozingatia maslahi ya wananchi wote.
Kwa mfano, kwa mujibu wa Makubaliano ya Muungano (Articles of Union), Rais wa Zanzibar anakuwa mmoja wa Makamo wawili wa Rais, na hivyo CUF inayachukulia Mabadiliko ya 11 ya Katiba ya Muungano kama ukiukwaji mkubwa wa Mkataba wa Muungano, na ambao unavunja misingi ya Muungano wenyewe. Sera ya CUF kuelekea Muundo wa Muungano ni Serikali Tatu, yaani ile ya Zanzibar, ya Tanganyika na nyengine ndogo ya Muungano.

Dira hii ya CUF inaweza kufanywa kuwa hai ikiwa kila Mtanzania ataungana na CUF kuihuisha. Jiunge sasa na ukombozi, saa ndiyo hii.

Nakala kamili ya toleo la Ijumaa hii la Annur

DONDOO MUHIMU
1 Hali za Masheikh mbaya Segerea
- Sheikh Mselem adhalilishwa vibaya
- Farid atoboa siri ya kukamatwa kwao
- Wamtaka Mwanasheria Mkuu wa Z’bar

2 Kuteswa Masheikh wasio na hatia…
Laana ya Siad Bareinatunyemelea
- Maafa Zanzibar, Dar huo ni mwanzo
- Makosa ya laana, balaa lake linakuja
- Toka lini ‘Alamtara’ ikawa kasida ya dufu?
3 Tusiparamie vikosi vya ATPU kama vile vya Uhuru Kenyatta
- Kasema kweli Askofu Lebulu
- Tusipojifunza kwa waliotangulia…
- Yakitukuta, tutulie, tusipige kelele
4 Saudia yadhihirisha kuipiga Yemen kwa niaba ya Marekani
5 Propaganda za udini shuleni Tanzania-2
- Na Profesa Ibrahim Noor Shariff
6 Nasaha kutoka kwa Jussa kwa vijana
7 Imebainika Saudia inashirikiana kijasusi na Israel
8 Kushutumiana kwenye mitandao sio maadili ya Uislamu
9 Mchango wa Waislmau katika maendeleo ya Dunia - 11
- Na Ben Rijal
10 Kuelewa moto katika Quran na mazingira
- Na Ben Rijal
11 Walimu wa Madrasa wameachiliwa - Katimba
- Madrasa zao sasa zafunguliwa
- Hakutakuwa na bughudha tena

Toleo la Ijumaa hii la gazeti la Annur


DONDOO MUHIMU
1 Tanzania, sasa kondoo anayesubiri kuchinjwa
- Magazeti yanalitoa Jini katika chupa…
- Polisi, JWTZ hawamuwezi subiani huyu

2 Hoja ni afya ya muunganosio umri wake- Awadh Said
3 Serikali yetu inasikitisha!
- Imezoeya kulea matatizo
- Wananchi wakikwama, nayo…Inakwama katika namna mbaya
4 Watoto wetu wanafundishwa Historia ya kughushi shuleni
- Ni kutokana na chuki za kidini
- Mzungu ageuzwa kuwa Muarabu
5 Tunahitaji wasomi wenye kuutambua ulimwengu wa leo
6 Ni nchi ya Wazanzibarisio ya wana-CCM, CUF
7 Siri kubwa ya vita Yemen yafchuka
- Mabeberu wamezea mate kisima cha mafuta
- Ni kikubwa zaidi duniani. Hakuna mfano wake
- Kiligunduliwa siku nyingi ikawa siri ya Marekani
- Rais kibaraka akaambiwa asiseme kwa wananchi
8 Tanzania na Propaganda za Udini
9 Mjue Abdurahman Ali Msham (mkombozi wa Tanganyika)
DONDOO MUHIMU
1 Tanzania, sasa kondoo anayesubiri kuchinjwa
- Magazeti yanalitoa Jini katika chupa…
- Polisi, JWTZ hawamuwezi subiani huyu

2 Hoja ni afya ya muunganosio umri wake- Awadh Said
3 Serikali yetu inasikitisha!
- Imezoeya kulea matatizo
- Wananchi wakikwama, nayo…Inakwama katika namna mbaya
4 Watoto wetu wanafundishwa Historia ya kughushi shuleni
- Ni kutokana na chuki za kidini
- Mzungu ageuzwa kuwa Muarabu
5 Tunahitaji wasomi wenye kuutambua ulimwengu wa leo
6 Ni nchi ya Wazanzibarisio ya wana-CCM, CUF
7 Siri kubwa ya vita Yemen yafchuka
- Mabeberu wamezea mate kisima cha mafuta
- Ni kikubwa zaidi duniani. Hakuna mfano wake
- Kiligunduliwa siku nyingi ikawa siri ya Marekani
- Rais kibaraka akaambiwa asiseme kwa wananchi
8 Tanzania na Propaganda za Udini
9 Mjue Abdurahman Ali Msham (mkombozi wa Tanganyika)

Wamasai wapewa Vitambulisho Zanzibar

 Na Jabir Idrissa

NINAONESHWA kwenye simu ya kisasa, nakala ya kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi chenye jina la kijana wa Kimasai, mkaazi wa mtaa wa Darajani, mjini Unguja. Anamiliki kitambulisho kilichotolewa Aprili 2015.

Hakuna mkweli anayeamini Darajani kuna Mmasai amezaliwa na leo afikie kuandikishwa kwenye orodha ya Wazanzibari wanaostahili kupewa kitambulisho hichi.

VIGOGO WA CUF WAANGUKA KWENYE KURA YA MAONI YA UBUNGE


MATOKEO ya awali ya kura za maoni kwa wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF) wanaowania Ubunge na Uwakilishi yameanza kutoka huku majina mapya yakichomoza kwa kupata ushindi dhidi ya wabunge Wanaotetea nafasi zao. 

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Nne wa Taifa

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Nne wa Taifa
Kwa mujibu wa matokeo ya awali yaliyopatikana mjini Unguja jana, Mbunge wa Gando, Khalifa Suleiman Khalifa (CUF), amebwagwa katika kura za maoni kwa kupata kura 81 dhidi ya Othman Omar Haji ambaye alipata kura 95 na Suleiman Salim Shukuru akiambulia kura saba. Mbunge wa Ole, Rajab Mbaruk Mohamed, amebwagwa wakati Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) akiangushwa na Sulemain Khalifan Saidi kwa tofauti ya kura mbili.
Mbunge wa Mkanyageni, Habib Mohamed Mnyaa, ameangushwa na Khamis Mohamed Khamis huku Mbunge wa Konde Hatib Said Haji akitetea nafasi yake kwa kupata kura 300 dhidi ya Mbunge aliyepita, Dk. Ally Tarab ambaye alipata kura 42 na Bakia Juma kura Saba. “Wabunge wengine walioshindwa katika kura za maoni ni Mbunge wa Mtambile, Masoud Abdallah Salim na Mbunge wa Magogoni Kombo, Khamis Kombo huku katika jimbo la Wawi aliyeshinda ni Waziri wa zamani wa SMZ, Juma Hamad Omari, ambaye alikuwa Waziri wa Utamaduni na Utalii wa Serikali ya Ali Hassan Mwinyi na kada wa CCM kwa wakati huo,” alisema mtoa habari wetu.
Kwa mujibu wa mapendekezo hayo, majina matatu yalipendekezwa kupigiwa kura ya maoni ngazi ya jimbo na wilaya kwa wagombea wa nafasi za viti maalumu kupata mgombea mmoja kabla ya kufanyika Uchaguzi Mkuu Oktoba 25 wa mwaka huu.

Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi wa CUF, Omar Ali Shehe alisema wanachama 517 walijitokeza kuwania ubunge, wakati 242 wanataka uwakilishi na 67 ni viti maalumu. Waandishi wa habari wanne walipenya katika hatua ya kwanza ya mchujo wa kutafuta wagombea.
Matokeo ya awali na kura za wagombea kwenye kwenye mabano zinaonyesha kama ifuatavyo;
Jimbo Kojani aliyeshinda ni Hamad Salim Maalim (198), Salim Yussuf Mohamed (57) na Haji Mussa Haji (54).
Uwakilishi katika jimbo hilo ni Salim Bakar Salim (128), Hassan Hamad Omar (113) na Hamadi Mussa Rashid (7).
Jimbo la Nungwi, Uwakilishi aliyepita ni Hassan Jani (144), Haji Mwadini (75) huku katika jimbo la Gando, Mbunge wa sasa Khalifa Suleiman Khalifa (CUF) amebwagwa katika kura za maoni kwa kupata kura 81 huku Othuman Omar Haji akipata kura 95 na Suleiman Salim Shukuru akiambulia kura 7.
Katika nafasi ya Uwakilishi, Said Ali Mbarouk (105), Ali Yusuf (50) na Kassim Hamad akiambualia patupu.
Jimbo la Magogoni, ubunge aliyeshinda ni Saleh Mohamed Saleh (48), Salum Mussa Haji (18) na Hamadi Ali Hamadi (37), huku Uwakilishi, Ali Hamad Ali (31), Rashid Hassan Rashid (13) na Maharouk Abdallah Suleiman (9).
Matokeo hayo ya awali yanaoyesha kuwa katika Jimbo la Mpendae, aliyeshinda kura za maoni ubunge ni Omar Mohamed Omar (23), Suleiman Khamis Ali (19) na Fakih Abdallah Pandu (9).
Jimbo la Chake chake, Uwakilishi, Omar Ali Shehe (106),
Ali Bakari (97) na Mohamed Subeit (27) huku jimbo la Nungwi, ubunge, Yussuf Haji Khamis (129), Juma Nyange Omar (68) na Vuai Ame Omar (31).
Kwa jimbo la Wete  Mbarouk Salim Ali (131), Seif Saleh Hamad (60) na Mwandini Abbas Jecha (30). Jimbo laKonde- Hatibu Said Haji (296), Dk. Ally Tarab (42) na Bakia Juma (7).
Jimbo la Mji Mkongwe, mbunge wa sasa, Muhammad Ibrahim Sanya (57), Mohamed Nur (29) na mwanahabari mkongwe visiwani na mtangazi wa BBC, Ali Saleh ‘Alberto’ (21).
Pia mkutano Mkuu wa jimbo hilo ulipga kura ya Ndiyo na Hapana baada ya mgombea wa nafasi ya Uwakilishi, Ismail Jussa Ladhu kukosa mpinzani.
Kura zilizompigia Ndiyo ni 79, zilizompigia Hapana ni 25 na nne ziliharibika.
Alipotafuwa, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CUF, Salim Biman, alisema hivi sasa wanaendelea kukusanya matokeo yote kwa mujibu wa utaratibu na yakikamilika itatolewa taarifa rasmi.
Kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi za CUF za jinsi ya kuwapata wagombea, atua inayofuata ni kwa Baraza Kuu la Uongozi la chama hicho ambacho ni chombo cha juu, kufanya uteuzi wa mwisho na kuamua nani atakuwa mgombea wake katika uchaguzi mkuu.
CHANZO: MTANZANIA

Vitambulisho vya Mzanzibari vyazua balaa Pemba


Na Mwandishi Wetu, Pemba

HALI ya siasa visiwani Zanzibar imeanza kuwa tete baada ya wabunge na wawakilishi wa Chama cha Wananchi (CUF), kuwaongoza wananchi katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mkoani kisiwani Pemba waweze kupewa vitambulisho vya Mzanzibari mkaazi.

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya tangazo lililotolewa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Hemed Suleiman Abdallah la kuwataka wabunge na wawakilishi kwenda kuwahamasisha wananchi wakachukue vitambulisho vyao.

Malumbano haya ya Maalim Seif na ZEC yanaitia doa Z’bar

Juzi, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad aliitisha mkutano na waandishi wa habari, Dar es Salaam na kutoa tuhuma nzito dhidi ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) akidai kuwa iliandikisha na kuruhusu watu wasiostahili zaidi ya 10,000 kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa 2010, kati ya hao, 8,507 wakiwa ni marehemu.
Maalim Seif, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CUF alidai kuwa wapigakura hao wasiostahili bado wapo kwenye Daftari la Kudumu la Wapigakura la Zanzibar.
Alitoa tuhuma hizo nzito alipokuwa akizungumzia utafiti wa Daftari la Kudumu la Wapigakura kwa Zanzibar uliofanywa na chama chake kati ya Agosti 2014 hadi Machi 2015.


Msichana aliyevunja ungo kisiasa


Ahmed Rajab Toleo la 405 13 May 2015
 
ZILZALA au Mapinduzi? Nini hasa kilichotokea Uskochi alhamisi iliyopita, Mei 8, wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Uingereza?

Pengine utauliza: yanatuhusu nini yanayojiri Uskochi iliyo masafa ya kilomita zaidi ya 7,000 na Tanzania? Ni swali halali. Jawabu la mkato ni kwamba jinsi ulimwengu ulivyokunjana siku hizi na kuwa mithili ya kijiji, hatuwezi kuyakwepa yanayotokea upande wa pili wa dunia. Hata kama tunataka kufanya hivyo, enzi hii ya digitali haitupi nafasi.

Tukitaka tusitake, tukipenda tusipende, tunajikuta tunayaangalia ya wengine.Tunayapima, tunayatathmini na tunayalinganisha na ya kwetu.

CUF DAR PRESS CONFERENCE MAZONGE YA ZECCM 10 MAY 2015

JUSSA: awanasihi vijana kujifunza kutoka kwa wazee

Ismail Jussa na Maalim Seif Sharif Hamad (pichani mwaka 1993) nyumbani kwa Maalim Seif, Mtoni Unguja.

NASAHA NJEMA KWA VIJANA WETU
Ismail Jussa

Nimeraghibika kuitumia picha hii leo kuwapa nasaha vijana wanaochipukia kupenda siasa na ambao wanadhihirisha uzalendo mkubwa kwa nchi yetu Zanzibar kwamba wasome na kukaa na wazee wenye hazina ya maarifa na historia ili waweze kuijua zaidi Zanzibar na pia kuongeza maarifa yao katika siasa na historia.

Maalim Seif na Fimbo ya Mussa

Na Ahmed Omar

Katika vitabu vyote vya dini kubwa duniani, kuna mkasa wa Nabii Musa aliyetumwa na Mungu kuwakomboa wana wa Israel kutoka utawala kandamizi wa Firauni. Firauni aliwatawala kama watumwa Waisraeli na akafanya vituko vingi duniani vya kukufuru hadi kufikia kujiita Mungu.

Mungu alimpelekea habari Firauni kwamba angelizaliwa mtoto wa kiume ambaye atakua nabii na kuleta nuru na ukombozi kwa watu wa Israel.

Baada ya kupata habari hizo, Firauni hakuruhusu uhai wa mtoto yeyote wa kiume aliyezaliwa akifahamu kwamba ndiye adui kwa utawala wake. Aliwaangamiza watoto wachanga wote wa kiume waliozaliwa ili kuunusuru utawala wake.

Jambo la kushangaza ni jinsi Nabii Mussa (mtoto wa kiume) alivyozaliwa mbali ndani ya kipindi hicho hicho na alivyokuja kulelewa na kukulia ndani ya kasri ya Firauni mwenyewe.

Hii ni kwa sababu Nabii Mussa ni rehma kutoka kwa Mungu, hivyo Firauni na wasaidizi wake hawakuwa na uwezo wa kumuangamiza. Nabii Mussa alikuwa yuko chini ya nusura ya Mungu ambayo bila shaka inashinda nguvu za wote ambao wangetamani kumdhuru.

Chini ya kivuli cha simulizi hiyo kutoka vitabu vitukufu, hebu tugeukie historia ya kisiasa ya Maalim Seif Sharif Hamad, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, ambayo inaonesha kwamba hakuwahi kabisa kutamani kuwa mwanasiasa wala kuwa kiongozi tokea utoto wake na ujana wake, ijapokuwa kipaji cha uongozi kilionekana kwake mapema mno.

Mnamo mwaka 1975, akiwa kwenye kazi yake ya ualimu katika chuo cha uwalimu Beit-el-Raas (sasa sehemu ya Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar, SUZA) alipokea wito kutoka Ofisi ya Rais, wakati huo Mzee Aboud Jumbe Mwinyi. Ikumbukwe kwamba wakati huo, ikiwa ndio kwanza ni muongo mmoja baada ya Mapinduzi na Muungano, na pia mwaka mmoja tu baada ya kuuawa kwa Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Sheikh Abeid Karume, nchi ilikuwa kwenye kipindi kigumu cha giza la kisiasa na kijamii. Kuitwa Ikulu hakukuwa na maana njema sana, katika hali ya kawaida.

Akiwa ameshangazwa na wito huo, kwa vile hakuwahi kuwa na mawasiliano wala mahusiano ya moja kwa moja na Ikulu, Maalim Seif aliitikia wito na Rais Aboud Jumbe akamwambia Maalim Seif kwamba kuanzia siku hiyo angelianza kufanya kazi katika ofisi yake kama katibu msaidizi maalum (special assistant) wa Rais. Hivyo ndivo rehema ya Mungu ilivyomfikisha Maalim Seif ikulu ya Zanzibar ndani ya zama za “sharia za kimapinduzi” (revolutionary justice). Hakuota, hakuwaza, hakujisogeza wala hakuomba.

Mwaka 1977, Rais Jumbe aliamua kufanya mabadiliko ya baraza la mapinduzi. Kupitia mabadiliko hayo alimtangaza Maalim Seif pamoja na wenzake kuwa ni mawaziri wapya wateule wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, yeye Maalim Seif akiwa ni waziri wa elimu.

Kufuatia mabadiliko hayo serikali ya Jumbe ikapata nuru. Ilitoa unafuu mkubwa kwa wananchi ukilinganisha na utawala wa Karume uliotangulia. Baada ya Mapinduzi, wanafunzi hawakuweza kuendelea na maomo kwa mujibu wauwezo wao wa kupasi mitihani bali ilikuwa kwa kuzingatia makabila ya baba zao. Utaratibu uliotumika uliruhusu Waafrika asilimia themanini (80%), Waarabu asilimia kumi na tano (15%), Wahindi asilimia nne (4%) na Wakomoro asilimia moja (1%) kuendelea na masomo.

Baada ya kuwa waziri Maalim Seif alimshauri Jumbe kuubadilisha utaratibu huo na badala yake wanafunzi wachaguliwe kuendelea na masomo kwa uwezo wao wa kupasi mitihani na sio makabila yao. Jumbe na Seif walifanikiwa kufanya hivyo, japokuwa walipambana na upinzani mkali wa akina Seif Bakari na Natepe waliokuwa wakijifanya kuwa waasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar (Burgess 2009).

Sambamba na hili Maalim Seif alifanya jitihada ya kuwatafutia wanafunzi wa Kizanzibari nafasi maalum za kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam hata kama kiwango chao cha kufaulu kilikuwa chini ukilinganisha na wanafunzi wa Tanzania Bara. Hoja ya Maalim Seif, kama waziri wa elimu, ilikuwa ni kwamba Zanzibar inatoa kiwango kidogo cha wanafunzi wanaokwenda katika elimu ya juu ukilinganisha na Tanzania Bara na kwa kuzingatia kwamba elimu ya juu ni suala la Muungano.

Maalim Seif pia alimshauri Rais Jumbe nafasi za elimu ya juu baina ya wanafunzi wa Pemba na Unguja iwe kwa uwiano wa asilimia 40 – Pemba na asilimia 60 – Unguja. Kabla ya hapo kulikuwa na kiwango kikubwa cha ubaguzi katika kuchagua wanafunzi wa kujiunga na vyuo vikuu baina ya Unguja na Pemba kukiwa na upendeleo mkubwa kwa kisiwa cha Unguja, ili kujenga chuki baina ya watu wa Unguja na Pemba. Hata hivyo, kutokana na asilimia kubwa (60) ya nafasi za Unguja, wanafunzi kutoka Unguja hawakuweza kujaza nafasi zao na hivyo nafasi hizo kukamilishwa na wanafunzi kutoka Pemba (Burgess 2009).

Baada ya Rais Jumbe kulazimishwa kujiuzulu mwaka 1984, Rais mpya Ali Hassan Mwinyi aliingia madarakani. Mwinyi alimteua Maalim Seif kuwa waziri kiongozi wa serikali yake. Chini ya ushauri mzuri wa Maalim Seif, Zanzibar ilizidi kupata neema katika utawala wa Mwinyi. Zanzibar ilirudisha matumizi ya paspoti ili kudhibiti uingiaji holela wa watu na hivyo basi mambo mengi ya udhia kama vile ujambazi, uhalifu, madawa ya kulevya na maradhi ya kuambukiza yaliweza kudhibitiwa.

Upigaji watu mikwaju kiholela na kuwaweka ndani mambo ambayo yalikuwa yakifanywa na Youth League katika awamu zilizotangulia yaliondoshwa. Serikali mpya pia ikawashawishi vijana kusoma na kupatiwa nafasi za masomo nje ya nchi. Halikadhalika vijana wasomi wakashawishiwa kuomba nafasi za uongozi serikalini, bila ya kuzingatia makabila ya baba zao au mahusiano ya baba zao na Uhizbu, Uafro au Ukomredi kama ilivyokuwa kabla (Burgess 2009).

Isitoshe, Mwinyi na Maalim Seif walianzisha katiba mpya ya mwaka 1984 iliyoruhusu utawala wa sheria na mipaka ya madaraka kwa mihimili ya dola ambayo iliandikwa na mwanasheria mkuu wa serikali wa wakati huo ambaye ni Waziri wa Katiba na Sheria wa sasa, Abubakar Khamis Bakar.

Vile vile, chini ya uongozi wa viongozi hao wawili, ulianzishwa mfumo mpya wa mahakama za kisheria na kufutilia mbali mahakama za wananchi zilizoanzishwa na Sheikh Karume ambazo zilikuwa zikiendeshwa kinyume na misingi ya sheria na haki. Haki za binaadamu katika katiba ya Zanzibar zililingana zaidi na zile zilizomo kwenye Tangazo la Haki za Binaadamu la Umoja wa Mataifa kuliko zile zilizokuwemo katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa kweli serikali ya Mwinyi na Maalim Seif pamoja na kudumu kwa muda mfupi sana, iliweza kuleta mabadiliko mengi. Mabadiliko mengine yalikuwa ni pamoja na uhuru wa wananchi kutoa maoni yao. Mambo mengi ambayo kwa njia moja au nyingine yalionekana kuwa ni ya kubana haki za raia ambayo yalikuja mara baada ya Mapinduzi, yalibadilishwa katika wakati huo. Vizuizi vingi vya kufaidi uhuru na haki za kiraia viliondolewa. Vyombo vya habari vya Serikali vilitakiwa kuanzisha vipindi maalum vya kuwapa nafasi wananchi kutoa maoni yao juu ya uendeshaji wa nchi yao. Vipindi kama ‘Zanzibar ni Njema’ katika Radio ya Zanzibar na ‘Jicho’ katika Televisheni ya Zanzibar (TVZ) vilivyotoa fursa kwa Wazanzibari kutoa maoni yao kuhusu uendeshaji na utendaji wa Serikali yao vilianzishwa katika kipindi hicho.

Lakini kubwa zaidi katika utawala wa Mwinyi na Maalim Seif ilikuwa ni kuruhusiwa biashara huria, yaani ‘Trade Liberalisation’ hatua ambayo ilipelekea ghafla kubadilika kwa hali za maisha ya watu na kuimarika kwa uchumi na pato la taifa. Jambo hili lilimchukiza sana Nyerere kwani ni kinyume na siasa yake ya ujamaa, lakini Mwinyi na Seif walimjibu Nyerere kuwa “tunataka kuuimarisha ujamaa kwa kutumia mfumo huria”. Majibu hayo yalimpoza Nyerere. Uhaba mkubwa wa chakula uliokuwepo kabla ulimalizika na umasikini ukapungua makali yake kwa kiwango kikubwa. Wafanyabiashara kutoka nchi za jirani kama Kenya na Tanzania Bara wakawa wanakuja Zanzibar kutafuta bidhaa. Maisha ya watu yakaboreka na neema kutanda. Hapo ndipo Mwinyi alipozaa msemo wake maarufu, Zanzibar ni njema atakae naaje na baadaye msemo huu ukawa miongoni mwa maneno ya hekima.

Huu ni upande mmoja wa hadithi ya mafanikio katika safari ya kisiasa ya Maalim Seif Sharif Hamad, ambayo ilidumu kwa kiasi ya muongo mmoja ndani ya serikali na Chama cha Mapinduzi (CCM). Lakini ukweli ni kwamba safari hii haikuwa nyepesi sana na kulikuwa na vigingi vingi ndani yake.

Baada ya kifo cha Edward Sokoine, Nyerere alimteua Salim Ahmed Salim kuwa waziri mkuu mpya. Hivyo basi Salim Ahmed Salim kwa upande wa Jamhuri ya Muungano alitarajiwa sana kuwa mrithi wa kiti cha urais baada ya kustaafu Nyerere.

Kwa upande wa Zanzibar nako Maalim Seif alitarajiwa sana kurithi kiti cha urais baada ya Mwinyi kumaliza muda wake. Upepo huo wa kisiasa haukuwa ukiwapungia vyema wanamapinduzi wa Zanzibar. Wanamapinduzi hawakupendelea mabadiliko hayo kutokea na walifanya kila wawezalo kuubalisha upepo huo wa kisiasa ili Salim Ahmed Salim kwa upande wa Jamhuri ya Muungano na Maalim Seif kwa upande wa Zanzibar wasiweze kuwa marais wanaofuatia.

Kosa la Maalim Seif lilikuwa ni Upemba wake, wakati Salim Ahmed alikuwa na makosa matatu kwa mujibu wa kamusi la kihafidhina la Zanzibar: Kosa la kwanza ni Uarabu, kosa la pili ni Upemba kama Maalim Seif na kosa la tatu ni mwanachama wa zamani wa ZNP.

Ijapokuwa Nyerere na Mwinyi walimuona Salim ndiye anayefaa zaidi kuwa raisi wa Jamhuri ya muungano, lakini alipigwa vita na wanamapinduzi.

Nyerere kwa kuwatii wanamapinduzi akasitisha azma ya kumteua Salim na badala yake akamteua Mwinyi kuwa rais mpya wa Jamhuri ya Muungano, baada ya yeye kung’atuka mwaka 1985. Kwa upande wa Zanzibar majina matatu ya Idri Abdul-wakil, Maalim Seif na Salmin Amour ndio yaliojadiliwa na Mkutano Mkuu wa CCM Taifa (NEC) kuteua mmoja wao kuwa rais mpya baada ya Mwinyi kupelekwa katika kiti cha urais wa Jamhuri ya Muungano.
Mzee Idris alikuwa wa mwanzo kuomba jina lake liondoshwe kutokana na uzee. Maalim Seif alikuwa kijana na alijulikana zaidi katika chama, katika NEC na wananchi wa Unguja na Pemba, hivyo kulikuwa na kila aina ya uwezekano wa kushinda kura nyingi kulinganisha na Idris Abdul-wakil. NEC ilishangazwa sana kutangazwa ushindi wa Idris Abdulwakil. Hapana shaka wanamapinduzi waliingilia kati suala hilo na kumfanya Nyerere kuchakachua matokeo ya kura ili kumpinga Maalim Seif na kumpitisha Idris.

Hapa ndipo wakati mgumu kwa siasa za Zanzibar baada ya kuzaliwa CCM ulipoanza. Wazanzibari hawakufurahia Mwinyi kupelekwa Bara wala hawakufurahishwa na uteuzi wa Idris na kuachwa Maalim Seif kwa kuwa Mzee Idris hakujulikana vyema na Wazanzibari.

Takriban asilimia 80 ya wananchi wa Pemba na asilimia 63 ya wanachi wa Mkoa wa Mjini Maghrib Unguja walimpigia Idris kura ya “hapana” na hivyo kuzua mtafaruku mkubwa wa kisiasa. Baada ya wimbi la kukataliwa Idris kutanda Zanzibar na hivyo siasa za CCM kuwa ngumu mno, Nyerere alimshauri Idris kumteua Maalim Seif kuwa waziri kiongozi. Lakini hata uteuzi huo wa waziri kiongozi haukuwafurahisha wanamapinduzi. Wao walitaka waziri kiongozi awe Salmin Amour. Hivyo basi wakazidisha na kuendeleza chuki na vita vyao dhidi ya Maalim Seif. Kila aina ya shutma na visingizio wakavitoa ili kumpotezea umaarufu Maalim Seif ndani ya chama na ndani ya serikali.

Moja ya shutma zilizowahi kutolewa ni kuwadharau, kuwavunjia heshima na kuwadhalilisha wanamapinduzi, akina Seif Bakari. Shutma nyengine ni kutaka kurejesha usultani Zanzibar.

Katika kipindi hichi kuliimarika mahusiano ya kidiplomasia baina ya Zanzibar na Falme za Kiarabu. Wanamapinduzi wakatumia fursa hiyo kutoa shutma kwamba Maalim Seif ana mipango wa kurejesha utawala wa kisultani Zanzibar.

Katika ziara moja ya Maalim Seif nchini Oman katika jitihada zake za kuiletea neema Zanzibar, Sultan Qaboos Busaid alisema wazi kwamba ana kila sababu ya kuisaidia Zanzibar kwa kiwango kikubwa kwa kuwa ni wasomi wa Kizanzibari ndio walioijenga Oman bila ya serikali ya Oman kuchangia chochote katika elimu zao (Burgess 2009).

Maalim Seif na Qabous kupitia ziara hiyo waliahidiana mambo mengi ya maendeleo kwa Zanzibar kama vile ujenzi wa viwanja vya ndege, kutanua miradi ya maji na ujenzi wa barabara. Ahadi zote hizo zilibezwa, kupuuzwa na kuzuiliwa utekelezaji wake na wanamapinduzi.

Tuhuma nyengine dhidi ya Maalim Seif ni kuwapendelea Wapemba. Maalim Seif alituhumiwa kuwapendelea wapemba kwa ushauri wake wa mgao wa huduma na mipango ya maendeleo kwa asilimia 60 kwa Unguja na 40 kwa Pemba. Baada ya tuhuma kadhaa wa kadhaa kushindikana kutumika kama sababu na visingizio vya kumtoa Maalim Seif katika wadhifa wake, ikatumika shutuma ya kufanya upinzani ndani ya chama. Kupokonywa Maalim Seif uwaziri kiongozi kukawadia na habari zikazagaa kila upande. Mrithi wa nafasi Maalim Seif iliamuliwa kuwa Dk. Omar Ali Juma ili kuwatuliza Wapemba baada ya kitendo cha kutolewa Maalim Seif.

Hata hivyo Dk. Omar aliposikia habari hizo haraka alifika kwa Maalim Seif na kumwambia kwamba kuna habari kwamba unataka kutolewa katika nafasi yako na baadae nafasi nipewe mimi, lakini mimi sitokubali nikijua ni kuwagawa Wazanzibari na kujenga fitna. Tarehe 18 Januari 1988, Seif Sharif akapokonywa wadhifa wa uwaziri kiongozi na Dk. Omar Ali Juma akachaguliwa kuwa waziri kiongozi mpya, huku Dk. Omar akifurahia na wala hakukataa kama alivyoahidi kabla.

Baada ya kitendo cha Maalim Seif kufukuzwa Zanzibar haikuwa shuwari. Mengi yalizungumzwa, chama cha CCM kulaaniwa na kukataliwa, Nyerere kuonekana ndiye anayewagawa Wazanzibari na Muungano kushutumiwa. Matukio hayo yalimkera sana Nyerere na ndipo alipolazimika kumfukuza Maalim Seif kabisa katika chama ili akose jukwaa la kufanyia siasa.

Kikao cha NEC kilichofuatia kilijadili tuhuma dhidi ya Maalim Seif na wenzake saba tuhuma dhidi ya Seif na wote walitakiwa kujiuzulu nafasi zao katika chama, ambapo baada ya wote kugoma kufanya hivyo Nyerere akatamka mbele ya wajumbe wa NEC “kama mmegoma kujiuzulu kwa nafasi niliyonayo nimekufukuzeni nyote katika chama”. Maalim Seif na wenzake walifukuzwa katika chama siku ya mwezi 27 Ramadhani, kwa mujibu wa Waislamu ni usiku wenye uwezekano mkubwa wa kupatikana lailatul-qadr.

Baada ya Maalim Seif kutolewa serikalini na kufukuzwa katika chama, Wazanzibari wakaghadhibika mno. Watu makundi kwa makundi wakarudisha kadi za chama na wengine kuzichana. Wengine walitengeneza sanamu za Nyerere, hususan huko Pemba, na kuziharibu hadharani kuonyesha hasira zao.

Mara tu Maalim Seif alipowasili kisiwani Pemba kutokea Dodoma makundi kwa makundi ya watu walikuwa wakikusanyika wakiwa na hamu na shauku ya kuzungumza nae. Nchi ilipooza na siasa za chama cha mapinduzi Zanzibar zikakwama. Nyerere akahisi kwamba hata kuwa nje ya chama na serikali, Maalim Seif ataendelea kuwa tishio kwa nchi na chama hivyo tuhuma kadhaa zikabuniwa ili kumtia gerezani.

Serikali ilijaribu kwanza kutaka kumshtaki Maalim Seif kwa madai kuiba nyaraka za serikali lakini baada ya kushindwa kuthibitisha walimshtaki kwa kosa la kuitisha mikutano haramu. Seif alifungwa jela kwa kipindi cha miezi 30 kuanzia mwezi wa Mei 1989 hadi mwezi wa Novemba mwaka 1991.

Jitihada mbali mbali zikachukuliwa za kidiplomasia, Shirika la Amnesty International na wasomi kudai Seif Sharif atolewe jela. Baada ya hapo akatolewa pamoja na masharti na vikwazo vingi. Pamoja na yote hayo bado Maalim Seif aliapa kutimiza ahadi yake ya kuwatetea Wazanzibari kama alivyoahidi. Na hilo ndilo ambalo amekuwa akifanya tangu wakati huo na hadi sasa. Mwalimu huyu ambaye hakuwahi kuwaza kama angekuwa kiongozi siku moja. Hii ina maana uongozi haikuwa tunu yake wala ndoto yake.

Tunaweza kusema uongozi kwa Maalim Seif ni rehma kwa Wazanzibari kutoka kwa Mungu ili aje awakomboe kutokana na utawala uliojengewa misingi imara kwa muda mrefu ya ubaguzi, chuki, farka, unyanyasaji, ukandamizaji na maonevu kadhaa wa kadhaa.

Maalim Seif ameletwa kuja kuwaunganisha Wazanzibari waliogawanywa tokea miaka ya 1950 na kuwafanya waonane kwamba wao ni ndugu wa damu. Maalim Seif amekuja kuwaunganisha Wazanzibari kudai nchi yao iliyopotea kupitia Muungano wa 1964 na kuirejesha ndani ya mamlaka yao ili waweze kujiamulia mambo yao yote kijamii, kisiasa na kiuchumi na hivyo wapate kuifaidi keki ya taifa lao tukufu.

Hivyo basi majemedari wa mapinduzi hawakuweza kuizuia rehema ya Mungu na hivyo hawakuwa na nguvu za kuiepusha rehma ya Mungu isimpeleke Maalim Seif ikulu ya serikali yenye misingi ya kimapinduzi. Viongozi wote wengine wanazuka, wanakuwa maarufu na kupotea, lakini sivyo kwa Maalim Seif ambae nyota yake inazidi kung’ara kila siku zikienda.

Jambo hili linawatahayarisha na kuwaiaibisha wale wote wenye mawazo ya akina Borafya Silima na Balozi Seif Ali Iddi ambao wanaodhani ipo siku wanaweza wakamtukana Maalim Seif akatukanika, wakamfedhehi akafedheheka, wakamkejeli akakejelika na wakamdharau akadharaulika. Kwa huyu haliwi, maana yeye ni mtu wa rehma kwa Wazanzibari na Zanzibar na wajiandae kumpisha akikalie kiti cha Utawala wa Zanzibar na awaletee wazanzibari maisha yenye utulivu wa nafsi sambamba na kiu yao ya muda mrefu ya haki, usawa na neema.
Chanzo:Mzalendo

Vitimbi vya CCM hawana mpya imepoteza dira na sifa za kuongoza


Salma Said, Zanzibar.
Wakati vyama vingi vinaanzishwa tena hapa Zanzibar vilianza na matumaini makubwa kutoka kwa wananchi baada ya kuchoshwa na ukiritimba wa chama kimoja. Matumaini makubwa yalitegemewa kupatikana kutokana na “chama tawala” kwamba kilikuwa tayari kujisahihisha na makosa yao ya nyuma na kutandika na kuonyesha njia na mwelekeo mpya wa kuongoza Taifa badala ya uchu wa kutawala.

Sababu zozote zile naziwe katika kuleta na hatimae kukubali mfumo wa vyama vingi mategemeo ya mabadiliko yalitarajiwa kuwepo na kuwepo kwa kiwango kikubwa pamoja na kusahau yaliyopita, ijapokuwa wengi walioathirika wamesamehe lakini hawakusahau.
Hali haikuwa hivyo bali ilikuwa kunyume chake ,chuki ,ubagizi ulizidi kushamiri na kupaliliwa.

MH ISMAIL JUSSA KATIKA CHUCHU FM

Jussa ziarani USA: Maswali na Majibu


 

Sitta akiwadanganya wana Diaspora wa US kama watoto wadogo.Sitta hafai, mpotoshaji, na mchochezi.

Maruhani hawakupindua Zanzibar

Ahmed Rajab
Toleo la 233
4 Apr 2012
SINA tabia ya kusutana, kubishana au hata kujibizana na wasomaji wa makala zangu wenye kutoa maoni tofauti na yangu. Ninaamini kwamba kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni yoyote ayatakayo hasa pale maoni hayo yanapokuwa ni ya ufafanuzi au uchanganuzi wa matukio ya kihistoria.
Kufanya ufafanuzi lakini ni tofauti na kuuelezea ukweli hasa ule ukweli wenye kuhusika na tendo ama vitendo fulani.
Nimekuwa nikisubiri kwa shauku kubwa hitimisho la makala za mwandishi mwenzangu wa Raia MwemaJoseph Mihangwa kumhusu John Okello.  Mfululizo huo wake wa makala zake kuhusu Okello na Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 ulikuwa ni majibu ya maandiko yangu juu ya mada ya Okello. Kwenye sahafu (safu) ya leo nataka kuyajibu baadhi ya yaliyomo kwenye majibu yake.
Kuna baadhi ya Wazanzibari wanaoona kwamba hakuna faida yoyote kujadili yaliyopita hasa sasa wakati wa mchakato wa Katiba mpya. Lakini wanakosea kwani tunaposonga mbele ni lazima tujue si tu hapa tulipo lakini pia tulikotoka. La sivyo tutajikuta tunajikwaa kila tunapopiga hatua.
Kuna tatizo kubwa kumtathmini Okello na dhima yake katika Mapinduzi ya Zanzibar. Sababu yake ni kuwako kwa simulizi zenye kukinzana kuyahusu Mapinduzi hayo na walioshiriki kwenye matukio yaliyoanzia Januari 12, mwaka 1964.
Migongano ya simulizi hizo yanamfanya mtu afikirie kwamba labda mapinduzi hayo yalifanywa na maruhani na kisha ndipo wanaadamu nao wakaingia. Ndio maana wengine chambilecho Sheikh Thabit Kombo, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Afro-Shirazi Party (ASP), wanaifikiria historia ya Zanzibar yote kuwa ni uongo mtupu. 
Lazima niseme hapa kwamba baadhi ya wanaotoa simulizi mbadala huwa hawana nia njema na Zanzibar. Simulizi zao huupotosha ukweli ili ziweze kuwa na mishiko. Mihangwa si miongoni mwao.  Yeye ni mwandishi mahiri mwenye kuandika baada ya kuridhika kuwa amefanya uchunguzi wa kina kuhusu mada inayohusika.
Nimekuwa nikiyafuatilia maandishi yake kuhusu Zanzibar kwa muda mrefu na kwa maoni yangu huyu ni mwandishi mwenye kutupenda laisa kiasi sisi wazawa wa Zanzibar. 
Lakini kwa vile yeye si mzaliwa wa Zanzibar na wala hajakuwako Visiwani (hasa Unguja) wakati wa Mapinduzi kwa kiwango kikubwa amekuwa akiwategemea wengine kwa masimulizi yake.  Pingine hao ndio waliompotosha.
Sitothubutu kusema kwamba ubara wake umeugubika utaalamu wake kwa sababu hakuteleza kuyaeleza ya Zanzibar tu kama alivyomuelezea Othman Sharif kuwa alikuwa Mkomunisti wakati bwana huyo akijulikana kwa chuki zake dhidi ya wenye siasa za mrengo wa kushoto.
Mihangwa ameteleza kwa mengine pia.  Kwa mfano, amemuelezea Idi Amin kuwa ni Mlangi, mtu wa kabila la Lango, ilhali tunajua kwamba alikuwa Mnubi wa kabila la Kakwa.
Tukiliacha hili la Okello, ambalo hakika Mihangwa halielewi, maandishi yake mengine kuhusu Zanzibar hayakirihishi kama ya wenzake wengi wa Bara. Mara kadha wa kadha kabla ya kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa huko Zanzibar alikuwa akiwavua nguo watawala wa Visiwani kwa kufuata kisiri siri sera za kibaguzi zilizopitishwa na Mkutano Mkuu wa ASP mwaka 1973 kule Pemba.
Kwa kiwango Fulani Mihangwa amesaidia kuwaelimisha Wabara wenzake kuhusu mgongano wa maneno na vitendo vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Juu ya hayo lazima tumkumbushe Mihangwa kwamba Che Guevara, mzawa wa Argentina, hakwenda Cuba kama mfanyakazi mhamiaji kama alivyokuwa Okello.   Che alikuwa msomi aliyeshirikiana na akina Fidel Castro, Raul Castro, Camilo Cianfuegos na Wacuba wengine waliokuwa uhamishoni kwenda Cuba kwa dhamira thabiti ya kufanya Mapinduzi ya kuikomboa nchi hiyo kutokana na udikteta wa Batista.
Wala Che hakuwahi kujaribu kudai na kupora haki ya kutawala na uongozi kama alivyofanya Okello  Zanzibar. Wacuba walimtunuku Che nyadhifa za uongozi  kwenye serikali yao mpya kwa ridhaa yao na kwa heshima kubwa. Walimfanyia hayo kwa vile walitambua mchango wake adhimu kwenye Mapinduzi yao.
Kiashiria kingine cha mapenzi ya Wacuba kwa Che ni pale Wacuba walipokwenda Bolivia alikouawa Che na kulisaka kaburi lake na kisha kuirejesha Cuba maiti yake kwa mazishi ya kitaifa.  Kumfananisha Che na Okello ni kumtukana Che bila ya kiasi.
Okello alionyesha chuki kubwa kwa Wazanzibari na kujisifu kwa kuwaua wengi mbali na kujaribu kupora hatamu za utawala kutoka viongozi wa ASP. Ukweli ni kwamba Okello anafaa kulinganishwa na jamaa yake Joseph Kony wa Lords Resistance Army ya kule Uganda na sio kumweka pamoja na Major Ernesto ‘Che’ Guevara.
Laiti Okello angalikuwa hai basi yakini angelijiunga na LRA kwani ni muumini wa dini ya Ukristo uchwara wa kuendesha mauaji ya kikatili sawa na mhalifu Kony.
Okello mwenyewe alizidi kuipotosha historia pale alipolalama kuwa Waafrika wa Zanzibar wamemfukuza baada ya yeye kwenda Visiwani kuwasaidia kuwashinda Waarabu waliokuwa wakiwachinja. Hapo ndipo tatizo linapoanza na hicho ndicho kielelezo au kiashirio cha uzushi unaobatizwa kuwa ‘historia ya nyumbani’.
Kwenye makala yake ya mwisho juu ya kadhia ya Okello, Mihangwa amemalizia kwa kuibua maswali muhimu kuhusu uhasama mkubwa uliojitokeza upande wa baadhi ya wakuu wa ASP dhidi ya Makomredi, yaani wafuasi wa Abdulrahman Babu na chama cha Umma Party.
Hii ni mada nzito lakini lazima tuigusie. Hali ya kutoaminiana kati ya Makomredi na wakereketwa wa ASP imekuwepo wakati wote chini kwa chini tangu kilipoundwa chama cha Umma Party mwaka 1963.
Juu ya kuwepo hali hiyo ilibidi pia wakati ule pawepo na aina ya ushirikiano kati yao katika kukabiliana na wapinzani wao yaani vyama vya Zanzibar Nationalist Party na Zanzibar and Pemba Peoples’ Party.
Haja hiyo ndiyo iliyopelekea pawepo umoja uliovishirikisha vyama vya ASP na Umma, vyama vya wafanyakazi pamoja na Jumuiya ya Wanafunzi.
Kiini cha kuwepo hali hiyo ya kutoaminiana ni ule msimamo wa itikadi ya kikabila wa takriban viongozi wote wa ASP wa kuwaepuka kisiasa Wazanzibari wenye asili ya kiarabu sembuse waliotokana na damu ya Hizbu. Mtazamo huu wa aina ya ‘kikaburu’ ndio uliokuwa msimamo na unaendelea hivyo hadi leo kwa upande wa wahafidhina wa iliyokuwa ASP.
Wabara wasioitakia kheri Zanzibar wamekuwa wakiipalilia moto hali hii iliwaweze kuidhibiti Zanzibar kwa maslahi yao. Kwa hiyo dhana ya Umma Party ya kuyasuka Mapinduzi ili yawe na mtazamo wa kitabaka pekee badala ya ‘ugozi’ (ubaguzi wa kikabila na wa rangi) ilisambaratishwa muda wote tangu kuanzia miaka ya mwanzo ya mwongo wa 1960 na akina Othman Sharif, Jamal Ramadhan Nasib na Mdungi Usi.
Baadaye usambaratishaji huo uliendelezwa na wanapinduzi kina Seif Bakari, Abdalla Said Natepe na kaumu yote ya ile ijulikanayo kama ‘Kamati ya Watu 14.’ Hao ndio waliomshinikiza Sheikh Karume kutowashirikisha Makomredi kwenye uongozi wa nchi.
Siku zote walikuwa wakimtisha Mzee Karume kuwa Makomredi walikuwa na njama na jamaa zao Wakiarabu za kuutokomeza utawala wa Waafrika. Hatimaye walifaulu pale Karume alipowatimua kutoka kwenye serikali kina Badawi Qullateinna Ali Sultan na kubwa lao Babu kudondoshwa na Julius Nyerere.
Kuna siku ambapo Brigadia Yusuf Himidi aliwasikitia baadhi ya wafuasi wa Umma Party waliokuwa naye kwa kuwaambia: “Eh jamaa fitna nyingi zimepita kutugombanisha.” Hakumtaja mtu lakini ilikuwa wazi kwamba mafatani walikuwa baadhi ya wahafidhina wa ASP.
Tatizo kubwa la Zanzibar ni kwa Wazanzibari kukubali kuhadaiwa na wanasiasa uchwara kuendelea kuwa wafungwa wa historia ya kisiasa iliyoigawa jamii katika makundi ya kikabila na kinasaba.
Jukumu linalotukabili sasa ni namna ya kutafuta njia za kuuyayusha urathi huu muovu unaoigawa jamii ya Wazanzibari na unaoutia sumu ufahamu au utambuzi wa pamoja wa Wazanzibari.
Okello alifurushwa Zanzibar kwa sababu alikuwa akileta matatizo. Alikuwa ni adha lakini hakuwa kitisho cha kisiasa. Angelikuwa ni  kitisho cha kisiasa basi isingekuwa rahisi kumng’oa nchini kama alivyotolewa.
Wala si peke yake kati ya wageni waliokuwa wakifanya fujo aliyefukuzwa Zanzibar. Mwengine alikuwa Engine kutoka Kenya.  Naye pia alitimuliwa baada ya kukamatwa huko Maruhubi, kwa amri ya Sheikh Karume, na kikundi cha Makomredi wakiongozwa na Ali Mshangama.
Mwengine aliyekuwa akiitwa Mfarinyaki alikamatwa Chwaka na Komredi Hamed Hilal aliyempeleka gerezani Kiinua Miguu.  Amri za kukamatwa Mfarinyaki aliitoa Yusuf Himidi akiwa mkuu wa jeshi.  Kwa nini hajawahusisha wanajeshi wengine na wapinduzi wa ASP, haijulikani.  Labda Yusuf Himidi alikwishang’amua kwamba wenzake walikosa nidhamu, wakijihusisha zaidi na wizi wa ngawira, wakati Makomredi walikuwa na nidhamu ya hali ya juu.
Hatujui pia kwa nini Karume alihiyari kuwatumia Makomredi kuwatimua akina Okello, Engine na wapinduzi wengine waliokuwa si wenyeji wa Zanzibar.
Yumkini Karume aliamua kuwatumia Makomredi kumfukuza Okello badala ya kuwahusisha akina Said Washoto, Mohamed Abdalla Kaujore, Seif Bakari, Khamis Darwesh na wengine wa Kamati ya Watu 14 kwa sababu alihisi wangelisitasita na pengine kuibua mgogoro. Said Abdallah Natepe aliwahi kuhadithia kwamba waliwahi kumjadili Okello miongoni mwao na hata pakatolewa wazo la kumuua. 
Sheikh Aboud Jumbe amekiri kwenye kitabu chake ‘The Part-nership’ kuwa alikuwa hawajui na hakupata kuwaona baadhi ya waliokuwemo kwenye  Kamati ya Watu 14, wakiwa pamoja na Okello.
Nakiri kwamba ni taabu kuamini ya kuwa Okello aliibuka ghafla Raha Leo kutoka halaiki ya watu waliokuwa wamekusanyika hapo.  Lakini pia tuna uhakika kwamba  Okello hakuwa na uwezo wala heshima anayobandikwa nayo na Mihangwa. 
Hatusemi hivi kwa sababu Okello hakuwa Mzanzibari.  Tunasema hivi kwa sababu huo ni ukweli huku tukikubali kwamba kuna haja ya kuiangalia upya nafasi yake Okello katika mchakato mzima wa maandalizi ya Mapinduzi.
Nimalizie kwa kukumbusha jingine.  Nalo ni kwamba kadhia niliyoieleza ya kutimuliwa Okello kutoka Zanzibar haikuwa ya mwanzo ya kufukuzwa Okello.  Mara ya kwanza alifukuziwa kutoka uwanja wa ndege wa Dar es Salaam na kusindikizwa hadi Nairobi na Oscar Kambona, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanganyika.
- See more at: http://raiamwema.co.tz/maruhani-hawakupindua-zanzibar#sthash.0FaflFge.dpuf
Ahmed Rajab Toleo la 233 4 Apr 2012

SINA tabia ya kusutana, kubishana au hata kujibizana na wasomaji wa makala zangu wenye kutoa maoni tofauti na yangu. Ninaamini kwamba kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni yoyote ayatakayo hasa pale maoni hayo yanapokuwa ni ya ufafanuzi au uchanganuzi wa matukio ya kihistoria.

Kufanya ufafanuzi lakini ni tofauti na kuuelezea ukweli hasa ule ukweli wenye kuhusika na tendo ama vitendo fulani.

Maruhani hawakupindua Zanzibar

Ahmed Rajab
Toleo la 233
4 Apr 2012
SINA tabia ya kusutana, kubishana au hata kujibizana na wasomaji wa makala zangu wenye kutoa maoni tofauti na yangu. Ninaamini kwamba kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni yoyote ayatakayo hasa pale maoni hayo yanapokuwa ni ya ufafanuzi au uchanganuzi wa matukio ya kihistoria.
Kufanya ufafanuzi lakini ni tofauti na kuuelezea ukweli hasa ule ukweli wenye kuhusika na tendo ama vitendo fulani.
Nimekuwa nikisubiri kwa shauku kubwa hitimisho la makala za mwandishi mwenzangu wa Raia MwemaJoseph Mihangwa kumhusu John Okello.  Mfululizo huo wake wa makala zake kuhusu Okello na Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 ulikuwa ni majibu ya maandiko yangu juu ya mada ya Okello. Kwenye sahafu (safu) ya leo nataka kuyajibu baadhi ya yaliyomo kwenye majibu yake.
Kuna baadhi ya Wazanzibari wanaoona kwamba hakuna faida yoyote kujadili yaliyopita hasa sasa wakati wa mchakato wa Katiba mpya. Lakini wanakosea kwani tunaposonga mbele ni lazima tujue si tu hapa tulipo lakini pia tulikotoka. La sivyo tutajikuta tunajikwaa kila tunapopiga hatua.
Kuna tatizo kubwa kumtathmini Okello na dhima yake katika Mapinduzi ya Zanzibar. Sababu yake ni kuwako kwa simulizi zenye kukinzana kuyahusu Mapinduzi hayo na walioshiriki kwenye matukio yaliyoanzia Januari 12, mwaka 1964.
Migongano ya simulizi hizo yanamfanya mtu afikirie kwamba labda mapinduzi hayo yalifanywa na maruhani na kisha ndipo wanaadamu nao wakaingia. Ndio maana wengine chambilecho Sheikh Thabit Kombo, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Afro-Shirazi Party (ASP), wanaifikiria historia ya Zanzibar yote kuwa ni uongo mtupu. 
Lazima niseme hapa kwamba baadhi ya wanaotoa simulizi mbadala huwa hawana nia njema na Zanzibar. Simulizi zao huupotosha ukweli ili ziweze kuwa na mishiko. Mihangwa si miongoni mwao.  Yeye ni mwandishi mahiri mwenye kuandika baada ya kuridhika kuwa amefanya uchunguzi wa kina kuhusu mada inayohusika.
Nimekuwa nikiyafuatilia maandishi yake kuhusu Zanzibar kwa muda mrefu na kwa maoni yangu huyu ni mwandishi mwenye kutupenda laisa kiasi sisi wazawa wa Zanzibar. 
Lakini kwa vile yeye si mzaliwa wa Zanzibar na wala hajakuwako Visiwani (hasa Unguja) wakati wa Mapinduzi kwa kiwango kikubwa amekuwa akiwategemea wengine kwa masimulizi yake.  Pingine hao ndio waliompotosha.
Sitothubutu kusema kwamba ubara wake umeugubika utaalamu wake kwa sababu hakuteleza kuyaeleza ya Zanzibar tu kama alivyomuelezea Othman Sharif kuwa alikuwa Mkomunisti wakati bwana huyo akijulikana kwa chuki zake dhidi ya wenye siasa za mrengo wa kushoto.
Mihangwa ameteleza kwa mengine pia.  Kwa mfano, amemuelezea Idi Amin kuwa ni Mlangi, mtu wa kabila la Lango, ilhali tunajua kwamba alikuwa Mnubi wa kabila la Kakwa.
Tukiliacha hili la Okello, ambalo hakika Mihangwa halielewi, maandishi yake mengine kuhusu Zanzibar hayakirihishi kama ya wenzake wengi wa Bara. Mara kadha wa kadha kabla ya kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa huko Zanzibar alikuwa akiwavua nguo watawala wa Visiwani kwa kufuata kisiri siri sera za kibaguzi zilizopitishwa na Mkutano Mkuu wa ASP mwaka 1973 kule Pemba.
Kwa kiwango Fulani Mihangwa amesaidia kuwaelimisha Wabara wenzake kuhusu mgongano wa maneno na vitendo vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Juu ya hayo lazima tumkumbushe Mihangwa kwamba Che Guevara, mzawa wa Argentina, hakwenda Cuba kama mfanyakazi mhamiaji kama alivyokuwa Okello.   Che alikuwa msomi aliyeshirikiana na akina Fidel Castro, Raul Castro, Camilo Cianfuegos na Wacuba wengine waliokuwa uhamishoni kwenda Cuba kwa dhamira thabiti ya kufanya Mapinduzi ya kuikomboa nchi hiyo kutokana na udikteta wa Batista.
Wala Che hakuwahi kujaribu kudai na kupora haki ya kutawala na uongozi kama alivyofanya Okello  Zanzibar. Wacuba walimtunuku Che nyadhifa za uongozi  kwenye serikali yao mpya kwa ridhaa yao na kwa heshima kubwa. Walimfanyia hayo kwa vile walitambua mchango wake adhimu kwenye Mapinduzi yao.
Kiashiria kingine cha mapenzi ya Wacuba kwa Che ni pale Wacuba walipokwenda Bolivia alikouawa Che na kulisaka kaburi lake na kisha kuirejesha Cuba maiti yake kwa mazishi ya kitaifa.  Kumfananisha Che na Okello ni kumtukana Che bila ya kiasi.
Okello alionyesha chuki kubwa kwa Wazanzibari na kujisifu kwa kuwaua wengi mbali na kujaribu kupora hatamu za utawala kutoka viongozi wa ASP. Ukweli ni kwamba Okello anafaa kulinganishwa na jamaa yake Joseph Kony wa Lords Resistance Army ya kule Uganda na sio kumweka pamoja na Major Ernesto ‘Che’ Guevara.
Laiti Okello angalikuwa hai basi yakini angelijiunga na LRA kwani ni muumini wa dini ya Ukristo uchwara wa kuendesha mauaji ya kikatili sawa na mhalifu Kony.
Okello mwenyewe alizidi kuipotosha historia pale alipolalama kuwa Waafrika wa Zanzibar wamemfukuza baada ya yeye kwenda Visiwani kuwasaidia kuwashinda Waarabu waliokuwa wakiwachinja. Hapo ndipo tatizo linapoanza na hicho ndicho kielelezo au kiashirio cha uzushi unaobatizwa kuwa ‘historia ya nyumbani’.
Kwenye makala yake ya mwisho juu ya kadhia ya Okello, Mihangwa amemalizia kwa kuibua maswali muhimu kuhusu uhasama mkubwa uliojitokeza upande wa baadhi ya wakuu wa ASP dhidi ya Makomredi, yaani wafuasi wa Abdulrahman Babu na chama cha Umma Party.
Hii ni mada nzito lakini lazima tuigusie. Hali ya kutoaminiana kati ya Makomredi na wakereketwa wa ASP imekuwepo wakati wote chini kwa chini tangu kilipoundwa chama cha Umma Party mwaka 1963.
Juu ya kuwepo hali hiyo ilibidi pia wakati ule pawepo na aina ya ushirikiano kati yao katika kukabiliana na wapinzani wao yaani vyama vya Zanzibar Nationalist Party na Zanzibar and Pemba Peoples’ Party.
Haja hiyo ndiyo iliyopelekea pawepo umoja uliovishirikisha vyama vya ASP na Umma, vyama vya wafanyakazi pamoja na Jumuiya ya Wanafunzi.
Kiini cha kuwepo hali hiyo ya kutoaminiana ni ule msimamo wa itikadi ya kikabila wa takriban viongozi wote wa ASP wa kuwaepuka kisiasa Wazanzibari wenye asili ya kiarabu sembuse waliotokana na damu ya Hizbu. Mtazamo huu wa aina ya ‘kikaburu’ ndio uliokuwa msimamo na unaendelea hivyo hadi leo kwa upande wa wahafidhina wa iliyokuwa ASP.
Wabara wasioitakia kheri Zanzibar wamekuwa wakiipalilia moto hali hii iliwaweze kuidhibiti Zanzibar kwa maslahi yao. Kwa hiyo dhana ya Umma Party ya kuyasuka Mapinduzi ili yawe na mtazamo wa kitabaka pekee badala ya ‘ugozi’ (ubaguzi wa kikabila na wa rangi) ilisambaratishwa muda wote tangu kuanzia miaka ya mwanzo ya mwongo wa 1960 na akina Othman Sharif, Jamal Ramadhan Nasib na Mdungi Usi.
Baadaye usambaratishaji huo uliendelezwa na wanapinduzi kina Seif Bakari, Abdalla Said Natepe na kaumu yote ya ile ijulikanayo kama ‘Kamati ya Watu 14.’ Hao ndio waliomshinikiza Sheikh Karume kutowashirikisha Makomredi kwenye uongozi wa nchi.
Siku zote walikuwa wakimtisha Mzee Karume kuwa Makomredi walikuwa na njama na jamaa zao Wakiarabu za kuutokomeza utawala wa Waafrika. Hatimaye walifaulu pale Karume alipowatimua kutoka kwenye serikali kina Badawi Qullateinna Ali Sultan na kubwa lao Babu kudondoshwa na Julius Nyerere.
Kuna siku ambapo Brigadia Yusuf Himidi aliwasikitia baadhi ya wafuasi wa Umma Party waliokuwa naye kwa kuwaambia: “Eh jamaa fitna nyingi zimepita kutugombanisha.” Hakumtaja mtu lakini ilikuwa wazi kwamba mafatani walikuwa baadhi ya wahafidhina wa ASP.
Tatizo kubwa la Zanzibar ni kwa Wazanzibari kukubali kuhadaiwa na wanasiasa uchwara kuendelea kuwa wafungwa wa historia ya kisiasa iliyoigawa jamii katika makundi ya kikabila na kinasaba.
Jukumu linalotukabili sasa ni namna ya kutafuta njia za kuuyayusha urathi huu muovu unaoigawa jamii ya Wazanzibari na unaoutia sumu ufahamu au utambuzi wa pamoja wa Wazanzibari.
Okello alifurushwa Zanzibar kwa sababu alikuwa akileta matatizo. Alikuwa ni adha lakini hakuwa kitisho cha kisiasa. Angelikuwa ni  kitisho cha kisiasa basi isingekuwa rahisi kumng’oa nchini kama alivyotolewa.
Wala si peke yake kati ya wageni waliokuwa wakifanya fujo aliyefukuzwa Zanzibar. Mwengine alikuwa Engine kutoka Kenya.  Naye pia alitimuliwa baada ya kukamatwa huko Maruhubi, kwa amri ya Sheikh Karume, na kikundi cha Makomredi wakiongozwa na Ali Mshangama.
Mwengine aliyekuwa akiitwa Mfarinyaki alikamatwa Chwaka na Komredi Hamed Hilal aliyempeleka gerezani Kiinua Miguu.  Amri za kukamatwa Mfarinyaki aliitoa Yusuf Himidi akiwa mkuu wa jeshi.  Kwa nini hajawahusisha wanajeshi wengine na wapinduzi wa ASP, haijulikani.  Labda Yusuf Himidi alikwishang’amua kwamba wenzake walikosa nidhamu, wakijihusisha zaidi na wizi wa ngawira, wakati Makomredi walikuwa na nidhamu ya hali ya juu.
Hatujui pia kwa nini Karume alihiyari kuwatumia Makomredi kuwatimua akina Okello, Engine na wapinduzi wengine waliokuwa si wenyeji wa Zanzibar.
Yumkini Karume aliamua kuwatumia Makomredi kumfukuza Okello badala ya kuwahusisha akina Said Washoto, Mohamed Abdalla Kaujore, Seif Bakari, Khamis Darwesh na wengine wa Kamati ya Watu 14 kwa sababu alihisi wangelisitasita na pengine kuibua mgogoro. Said Abdallah Natepe aliwahi kuhadithia kwamba waliwahi kumjadili Okello miongoni mwao na hata pakatolewa wazo la kumuua. 
Sheikh Aboud Jumbe amekiri kwenye kitabu chake ‘The Part-nership’ kuwa alikuwa hawajui na hakupata kuwaona baadhi ya waliokuwemo kwenye  Kamati ya Watu 14, wakiwa pamoja na Okello.
Nakiri kwamba ni taabu kuamini ya kuwa Okello aliibuka ghafla Raha Leo kutoka halaiki ya watu waliokuwa wamekusanyika hapo.  Lakini pia tuna uhakika kwamba  Okello hakuwa na uwezo wala heshima anayobandikwa nayo na Mihangwa. 
Hatusemi hivi kwa sababu Okello hakuwa Mzanzibari.  Tunasema hivi kwa sababu huo ni ukweli huku tukikubali kwamba kuna haja ya kuiangalia upya nafasi yake Okello katika mchakato mzima wa maandalizi ya Mapinduzi.
Nimalizie kwa kukumbusha jingine.  Nalo ni kwamba kadhia niliyoieleza ya kutimuliwa Okello kutoka Zanzibar haikuwa ya mwanzo ya kufukuzwa Okello.  Mara ya kwanza alifukuziwa kutoka uwanja wa ndege wa Dar es Salaam na kusindikizwa hadi Nairobi na Oscar Kambona, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanganyika.
- See more at: http://raiamwema.co.tz/maruhani-hawakupindua-zanzibar#sthash.0FaflFge.dpuf
Ahmed Rajab
Toleo la 233
4 Apr 201
Ahmed Rajab
Toleo la 233
4 Apr 201
Ahmed Rajab
Toleo la 233
4 Apr 201
Ahmed Rajab
Toleo la 233
4 Apr 201

HABARI ZILIZOJIRI LEO


Topics :
 
Support : ZENJIBARZA
Copyright © 2011. ACT WAZALENDO DIASPORA NETWORK - All Rights Reserved