Headlines News :
KARIBU CUF DIASPORA NETWORK - CUF HAKI SAWA KWA WOTE...TEGEMEA KILA JIPYA NA ZURI KUTOKA KWETU...LIKE PAGE YETU KWENYE FACEBOOK
Showing posts with label MAKALA. Show all posts
Showing posts with label MAKALA. Show all posts

CUF Wanawake wawapa 'take-care' Mutungi, Lipumba


Huku wakisubiri hukumu ya kesi zao zilizoko mahakamani dhidi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, na Profesa Ibrahim Lipumba, Jukwaa la Wanawake la CUF linamuonya Jaji Mutungi kuwa pakitokezea lolote baya kwenye nchi atahusika moja kwa moja


 

NDUNGAI NI NYOKA ANETAFUNA MKIANI

SERIAKLI YA CCM INAVYOJIKANYAGA LIPUMBA NA SAKAYA SIO WANCHAMA WA CUF ni mamluki walionunuliwa na CCM kuisambaratisha CUF kwa k usaidiwa na Msajili wa vyama , BRELA na Ofisi ya Speaker kutumika kuvuruga demokrrasia na kuzuia mabadiliko ndani ya nchi

Katibu Mkuu wa Chama cha CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amesema kwamba hatua ya Spika kuwavua ubunge , udiwani na kuteua wengine wapya inalenga kudhoofisha kambi ya wabunge wa CUF na Ukawa. Amesema Watanzania wanapaswa wajikumbushe kwamba hata kama hicho kinachoitwa ‘kuwafukuza uanachama’ wabunge halali wa CUF kingekuwa kiko sawa, hatua kama hiyo hufuata taratibu zote za kisheria na kikanuni za Bunge kujiridhisha kwanza. “ Spika Job Ndugai anadhani Watanzania ni vichaa wamuamini kuwa alishachukua hatua ya kujiridhisha kuwa wabunge wanane wa Chama cha Wananchi (CUF) wamefukuzwa uanachama kulingana na taratibu za chama hicho na hivyo wamekosa sifa za kuendelea na Ubunge. Ndani ya siku moja?” amehoji Maalim. Ameongeza kuwa Spika amejiridhisha vipi ikiwa hata hakuwasiliana na Katibu Mkuu wa Chama ambaye kwa mujibu wa Katiba ya CUF ndiye Mtendaji Mkuu wa shughuli za chama na pia kwa nafasi hiyo ndiye katibu wa vikao vya Mkutano Mkuu wa Taifa na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama? Amesema yeye kama katibu, alimuandikia Spika Ndugai barua, Jumanne, Julai 25 akimueleza kwamba hilo lililoitwa Baraza Kuu la Uongozi la CUF halikuundwa na wajumbe halali wa Baraza Kuu. “Angekuwa na nia ya kweli ya kutaka kujiridhisha si hapo ndipo pangekuwa pa kuanzia kwa kuwepo kile wanasheria wanachokiita shaka inayoweza kuingia akilini yaani ‘reasonable doubt’?’’ amehoji. Hata hivyoa amesema Spika Ndugai aliyapuuza yote hayo kwa sababu ni kinyume na mkakati wa Dola wa kuihujumu CUF na kuua demokrasia Tanzania. Hapo ndipo Spika Job Ndugai alipolifikisha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

MAHAKAMA YAIPIGA NA CHINI HOJA ZA SERIKALI DHIDI YA KESI YA CUF

Mahakama yatupa hoja za serikali ya kesi ya CUF


MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imekubaliana na hoja za Wakili wa Wabunge wanane wa Chama cha Wananchi CUF ambao ubunge umetenguliwa baada ya kuvuliwa uanachama, na sasa pingamizi la muda litaanza kusikilizwa Jumatatu,


Awali serikali iliwasilisha mapingamizi matatu ambapo jana iliondoa moja na kubakia mawili likiwamo la kuiomba mahakama isiingilie mhimili wa Bunge kwa kuzuia wabunge hao wasiapishwe.
Mapingamizi mawili ya serikali nayo yalitupwa na mahakama huku serikali ikiambiwa kinachofanyika siyo kuingilia mhimili wa Bunge.
Kwa mujibu wa mahakama, shauri dogo namba 479 litaanza kusikilizwa jumatatu ambalo litakuwa na mambo makuu saba likiwamo hoja ya kuzuia wabunge wanane wa CUF kuapishwa.

Jaji Lugani Mwandambo amekubali hoja za Wakili wa wabunge hao, Peter Kibatala kwamba shauri hilo limefunguliwa kwa kifungu sahihi na kwamba litaendelea kusikilizwa.

Mahakama hiyo imezitupa hoja tatu za serikali, ikiwamo kutaka chombo hicho kutupilia mbali hoja za kuzuia kuapishwa wabunge hao.Mwandambo alisema kinachofanyika kwa sasa katika kesi hiyo siyo kuingilia mahakama kama hoja ya serikali ilivyowasilisha hoja hiyo.

Chanzo cha wabunge hao kuvuliwa ubunge kimetokana na Chama cha Wananchi (CUF), chini ya Profesa Ibrahim Lipumba kuwavua uanachama.*

MAAAMUZI YA BARAZA KUU LA UONGOZI LA TAIFA LA THE CIVIC UNITED FRONT (CUF - CHAMA CHA WANANCHI) KUHUSIANA NA HUJUMA ZA DOLA DHIDI YA CUF

Image may contain: 1 person
BARAZA Kuu la Uongozi la Taifa lilipokea, kujadili na kufanya maamuzi kuhusu ajenda moja tu iliyowasilishwa kwake na Kamati ya Utendaji ya Taifa ambayo ilikuwa ni: • Taarifa kuhusu kile kinachoitwa kuwavua uanachama Wabunge wanane (8) na Madiwani wawili (2) wa Viti Maalum kupitia CUF kilichotangazwa kufanywa na Ibrahim Lipumba na kikundi chake ikiwa ni mwendelezo wa hujuma za Dola dhidi ya Chama cha CUF. Baada ya mjadala wa kina, Baraza Kuu la Uongozi la Taifa linapenda kutoa maazimio yafuatayo kuhusiana na tukio hilo na mwendelezo wa vitendo na matukio mengi ya hujuma yanayofanywa na Dola dhidi ya CUF:-

1. KUHUSU UHALALI WA BARAZA KUU LA UONGOZI LA TAIFA: Kutokana na mkanganyiko unaosababishwa na upotoshaji wa makusudi unaofanywa na Ibrahim Lipumba na kikundi chake wa kuitisha watu wa kuokota barabarani na kuwakusanya Buguruni huku akiwaita kuwa ndiyo Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la CUF, tumeona kuna haja ya kuweka kumbukumbu sahihi ili kuepusha upotoshaji huo usiendelee. Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama huwa linaundwa kila baada ya miaka mitano kupitia Uchaguzi Mkuu wa Chama ndani ya Chama na hupata wajumbe wake kupitia uchaguzi unaofanywa na Mkutano Mkuu wa Taifa (wajumbe 25 kutoka Tanzania Bara na wajumbe 20 kutoka Zanzibar), wajumbe 14 wanaoteuliwa na Mwenyekiti kwa kushauriana na Makamu Mwenyekiti na kisha kuthibitishwa na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa, wajumbe wanaoingia kwa nafasi zao wakiwemo Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Chama, Wenyeviti na Makatibu wa Jumuiya za Chama na Viongozi wa Kambi za Wabunge na Wawakilishi wa Chama. Viongozi Wakuu wa kitaifa wa Chama pia ni wajumbe. Wafuatao ndiyo Wajumbe halali waliochaguliwa na Mkutano Mkuu wa Taifa uliomalizika Juni 27, 2014 hapo Ubungo Plaza, Dar es Salaam kuwa wajumbe wa Baraza Kuu la Uongozi la Taifa (BKUT) watakaokaa madarakani kwa kipindi cha miaka mitano (2014 – 2019) hadi watakapochaguliwa wengine na Mkutano Mkuu wa Taifa kwa mujibu wa Katiba ya CUF ya mwaka 1992 (Toleo la 2014):- VIONGOZI WAKUU: 1. Mwenyekiti (alijiuzulu tarehe 5 Agosti, 2015 na kujiuzulu kwake kuthibitishwa na Mkutano Mkuu wa Taifa wa dharura tarehe 21 Agosti, 2016).

Mbunge wa Temeke akamatwa kihuni

Image result for ABDALL MTOLEA PICTURES

SITAKI KUMUONA LIPUMBA ASEMA MBUNGE WA TEMEKE

Mbunge wa Temeke kwa tiketi ya CUF, Abdallah Ally Mtolea amefunguka na kusema kwa sasa hana jambo la kumshauri Profesa Lipumba na kudai haitaji hata kumuona kwa sababu ameshapoteza ile heshima na thamani yake.

Mtolea amesema hayo leo alipokuwa akihojiwa na EATV na kusema yeye alikuwa ni miongoni mwa watu ambao walikuwa wanamuheshimu sana  Prof. Ibrahim Lipumba kiasi kwamba ilifika hatua hakutaka kua muongeaji sana juu ya mambo yake lakini kwa kuwa tayari ameshajivunjia heshima mwenyewe hivyo hana budi kusema.
"Mimi nilianza kuona nia mbaya ya Lipumba pale aliponikatalia kwenda kwenye ufunguzi wa kampeni zangu mwaka 2015 kwani nilimfuata lakini yeye alikataa kabisa, lakini niliposhinda ubunge nilimfuata pia na kumpa taarifa na kumuomba tuendelee kushirikiana nikiamini yeye ni mkongwe katika siasa kuna mambo mengi ya kunishauri na kuniongoza sikumtenga kabisa, ila aliposema anataka kurudi baada ya kujiuzulu mimi sikumuelewa ni nikamfuata nikimwambia mzee unataka kutuletea mgogoro" alisema Mtolea 
Mbali na hilo Mtolea anasema saizi Lipumba amefikia hatua ambayo haambiliki chochote na kusema hatamani hata kukutana naye 
Msikilize hapa akifunguka zaidi 

Kesi YA CUF DHIDI YA RITA KUUNGURUMA JULAI 10

 

Mashauri sita yaliyofunguliwa katika Mahakama Kuu na Bodi ya Wadhamini ya CUF yanatarajiwa kusikilizwa na baadhi yake kutajwa tarehe, Jumatatu ya Julai 10, 2017, baada ya leo kuahirishwa usikilizwaji wa kesi ya msingi ya wizi wa ruzuku ya chama hicho. Kufuatia mawakili upande wa mashitaka kutopewa nakala ya maombi ya pingamizi la Mwanasheria Mkuu wa Serikali. 
Wakati akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya kuahirishwa kwa kesi hiyo, Wakili wa CUF, Juma Nassoro amesema leo mahakama hiyo imewapatia nakala za pingamizi hilo.
Na kwamba, Jaji Wilfred Dyansobela anayesimamia mashauri hayo amesema Jumatatu ijayo mashauri yote yatasikilizwa na kutajwa tarehe ikiwemo la kupinga maamuzi ya RITA ya kusajili wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Profesa Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti CUF anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa .
Shauri lingine litakalosikilizwa siku hiyo ni la kuzuia fedha za ruzuku ya chama hicho kupewa Profesa Lipumba na wenzake.
Aidha, upande wa Lipumba kupitia Abdul Kambaya haikuridhishwa na maamuzi hayo ya mahakama ya kuahirisha usikilizwaji wa kesi hiyo ya msingi kwa madai kuwa yanachelewesha muda.
“Sisi tulikuja kwa agizo la mahakama, badala yake jaji hakutokea tukasikia juu kwa juu kuwa kesi imeahirishwa. Wanachokifanya ni kuchelewesha muda jumatatu watazikwa,” amesema.  

TAMKO LA MADIWANI WA THE CIVIC UNITED FRONT (CUF-CHAMA CHA WANANCHI) WA MKOA WA DAR ES SALAAM JUU YA KUUNGA MKONO HOTUBA NA MSIMAMO WA CHAMA ULIOTOLEWA NA KATIBU MKUU MAALIM SEIF SHARIF HAMAD TAREHE 28 JUNE 2017 KATIKA HOTEL YA PEACOCK:

4
Image may contain: 4 people, people sitting, table and indoor
THE CIVIC UNITED FRONT
(CUF-CHAMA CHA WANANCHI)
TAMKO LA MADIWANI WA THE CIVIC UNITED FRONT (CUF-CHAMA CHA WANANCHI) WA MKOA WA DAR ES SALAAM JUU YA KUUNGA MKONO HOTUBA NA MSIMAMO WA CHAMA ULIOTOLEWA NA KATIBU MKUU MAALIM SEIF SHARIF HAMAD TAREHE 28 JUNE 2017 KATIKA HOTEL YA PEACOCK:
Tarehe 5 JULY, 2017
NDUGU WAANDISHI WA HABARI,
WAHESHIMIWA VIONGOZI WA CUF,
WAHESHIMIWA WANACHAMA WA CUF,
WAHESHIMIWA WANANCHI, MABIBI NA MABWANA,
NAOMBA NIANZE KWA KUWASALIMU KWA SALAMU ZA CHAMA CHETU HAKI SAWA KWA WOTE,
1. Awali ya yote, tuanze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kutujaalia uhai na uzima na kutuwezesha kukutana hapa asubuhi hii, kwa lengo la kutoa Tamko na msimamo wetu Rasmi juu ya sintofahamu inayoendelea ndani ya Chama chetu, na kuunga mkono Hotuba na msimamo wa Chama uliotolewa na Katibu Mkuu wetu, Maalim Seif Sharif Hamad. Tukiwa ni Madiwani wa CUF, kutoka Manispaa za Mkoa wa Dar es Salaam na kupitia kwenu ujumbe wetu uweze kuwafikia wana-CUF wenzetu, Wapenda Mabadiliko wote nchini, na Watanzania kwa Ujumla.
2. Tunapenda kuchukua fursa hii kuwashukuru nyinyi Waandishi wa Habari kwa kuhudhuria kwenu na mara zote kutukimbilia kila tunapokualikeni mbali na Changamoto mnazokabiliana nazo juu ya uhuru wa Habari na aina ya uongozi wa Serikali ya awamu ya Tano jinsi unavyoikandamiza demokrasia nchini na kutopenda kukosolewa.

ZANZIBAR STONE TOWN MEMBER OF PARLIAMENT STAND WITH GIRLS

I STAND FOR THE GIRLS ... PLEASE JOIN ME
Image result for ALLY SALEH PICTURES
By Ally Saleh
Many people have come to the defence of young girls who get into wrong side and become pregnant while still at school be it at primary level or secondary one and thus cut off from following their educational programs.
Thus means not only dreams but also hopes are dashed and buried in a grave that most of them would not be able even to trace as they grow old and lament only. But then lamenting will not be enough because their lack of education might be an obstacle to their development and end up in the poverty cycle.
Most people believe that pregnancy in young girls is never wanted but these young females are caught at a time when they are not only naïve but also at an age where foolishness is only thing they do. And on top of it both young men and those of old age with good cash flow pry on these innocent souls and and trap them.
Some feel it is cruel to blame a girl of 13 or even 16 and 17 to have willingly made a choice of entering sex life and hence with no education to protect herself from becoming pregnant but even from being passed with HIV AIDS or any other sexual transmitted diseases.
A month ago a debate ensued at the Parliament about change of the 1971 Law of Marriage Act in order to change marriage age in Tanzania and a big shout was recorded with two opposing sides arguing their cases with no results. Those who refuse lean on morality and those who want it be raised to be 18 lean of reality.
There not even consensus with the Cabinet Members as the then newly appointed Minister for Constitutional and Legal Affairs Professor Palmagamba Kabudi took a cautious approach saying the government was still synthesizing the issue while Minister for Women and Health Ummy Mwallimu skipping out of official Budget presentation notes indicated that things were moving on to effect changes.
But while the debate is still raging in the public domain with consensus being sought with activists charging time was up for the changes, the traditionalist especially those with religious inclinations have been saying this was only going to happen over their dead bodies.
The latter’s argument is that if a girl was pregnant and returned to classes after delivery will poison the others on their habits, which tends to assume that the only bad thing is to become pregnant ignoring the very act of having sex which is not committed only by the girl who becomes pregnant but many and most others around her.

BODI FEKI YA LIPUMBA YA GONGA MWAMBA

UPDATES KUTOKA MAHAKAMA KUU LEO TAREHE 29/6/2017



MAHAKAMA YAPANGA KUSIKILIZA PINGAMIZI LA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI:

Leo mbele ya Mheshimiwa Jaji Wilfred Dyansobera amefanya maamuzi ya kuahirisha Shauri la Msingi Miscellaneous Civil Cause No. 21/2017 kuhusu wizi wa shilingi milioni 369 fedha za Ruzuku za Chama cha CUF uliofanywa na Lipumba na genge lake wakishirikiana na Msajili wa Vyama vya siasa nchini Jaji Franscis Mutungi mpaka Tarehe 6 July, 2017. Maamuzi hayo yameelezwa mbele ya Mahakama ya wazi (Open Court) iliyofurika wana NGANGARI wakiongozwa na Wabunge 40 wa CUF na kikosi makini cha ulinzi wa Chama Blue Guards. Hatua hiyo imefikiwa baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (Senior State Attorney) Wakili Msomi SILVESTER MWAKITALE – kuiomba Mahakama kuhairisha shauri hilo ili waweze kuwapatia nakala za Pingamizi (Copy of Preliminary Objection to be saved to Applicant-(THE REGISTERED TRSTEES OF THE CIVIC UNITED FRONT (CUF-CHAMA CHA WANANCHI). Upande wa Mawakili wasomi wa CUF ukiongozwa na JUMA NASSOR, HALFANI DAIMU NA HASHIMU MZIRAY ulikuwa hauna Pingamizi na Maombi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya kuweka pingamizi hilo na kukubaliana na kuagizwa na Mahakama kuwa kesho Tarehe 30/6/2017 nakala hizo wapatiwe Mawakili wa CUF na pingamizi hilo litasikilizwa Tarehe 6 July, 2017.

Katika hatua nyingine Mahakama Kuu haikuweza kufanyia kazi Maamuzi yake iliyoyatoa awali Shauri lilipoitwa mbele ya Jaji Tarehe 21/6/2017 juu ya kuwataka kufika Mahakamani Afisa wa RITA na Thomas Malima aliyejitambulisha kama Katibu wa Bodi ya Wadhamini aliyewasilisha barua ya kutaka Kufuta kesi zote zilizopo Mahakamani hapo kuleta ushahidi na kuthibitisha nyaraka zilizowasilishwa Mahakamani za kuteuliwa kwa ‘Bodi FEKI’ ya Wadhamini na pia kutaka kuwaondoa mawakili wanaoiwakilisha Bodi Halali ya Wadhamini ya CUF pamoja na kutaka kumuingiza Wakili Mpya atakaye iwakilisha ‘Bodi FEKI’ ya Lipumba na genge lake Mhe. Makubi Makubi. Kutosikilizwa kwa suala la maombi ya kufuta kesi limetokana na uwepo wa pingamizi la Mwanasheria Mkuu wa Serikali na hivyo kuamuriwa kuwa masuala hayo yatajadiliwa baada ya pingamizi hilo kusikilizwa na kutolewa maamuzi ndipo itaangaliwa kama kuna haja ya kuendelea na maombi hayo ya kufuta kesi hizo.

Mahakama Kuu imeendelea kuwatambua Mawakili wa Bodi Halali ya Wadhamini wa CUF inayoongozwa na Katibu Mkuu Maalim Seif Sharif Hamad na kuiweka pembeni barua ya ‘Bodi FEKI’ ya Genge la Lipumba kutaka kubadilisha mawakili hao kwa kumuingiza wakili wao. Leo mawakili wa Lipumba na genge lake hawakuruhusiwa kushiriki katika kesi hiyo kwa kuwa si sehemu ya walalamikiwa (Respondents). Kesi hii inawahusu Bodi ya Wadhamini-CUF dhidi ya Mutungi na Mwanasheria Mkuu wa serikali.

Wakati huohuo CUF IKIWA NI TAASISI IMARA, YENYE VIONGOZI MAKINI tayari imeshachukua hatua za kutekeleza Maazimio ya Kikao Cha Kamati ya Utendaji Taifa kilichofanyika tarehe 23/6/2017 na kuongozwa na Mwenyekiti wake Maalim Seif Sharif Hamad katika Ofisi ndogo ya Makao Makuu Vuga, Zanzibar kushughulikia kisheria kuipinga Bodi FEKI ya lipumba kwa mujibu wa Sheria ya REGISTRATION INSOLVENCY AND TRUSTEESHIP AGENCY (RITA) THE TRUSTEES INCORPORATION ACT [CAP 318-R.E 2002] AN ACT TO PROVIDE FOR THE INCORPORATION OF CERTAIN TRUSTEES.

Article 26. “Application to decide question whether a person is a member of a corporate body or as to property When any question arises as to whether a person is a member of a body corporate or as to the vesting or divesting of any property under the provisions of this Act, any person interested in such question may apply to the High Court for its opinion on such question and notice of hearing shall be given to such persons and in such manner as the court shall think fit, and any opinion given by the court on an application under this section shall be deemed to have the force of a declaratory decree.” [s. 18]

Sheria hii inaeleza wazi kuwa “…kama kuna mtu yeyote ambaye hakuridhika na maamuzi ya RITA kuteua wajumbe wa Bodi ya Wadhamini sheria inampa haki ya kufungua mashtaka Mahakama Kuu na kupinga maamuzi ya RITA. Maamuzi ya Mahakama Kuu ndiyo yatakayo zingatiwa na kufuatwa kwa kuwa na nguvu ya kisheria.”

Pamoja na hilo wahusika wote walioshiriki kufoji nyaraka watapaswa kuitwa mbele ya Mahakama Kuu na kujibu kwanini wasitiwe hatiani na Kufungwa Jela kwa makosa hayo.

HAKI SAWA KWA WOTE

SALIM BIMAN
MKURUGENZI WA HABARI, UENEZI NA MAHUSIANO NA UMMA CUF-TAIFA
ZANTEL-0777414112
VODA-0752325227

MBARALA MAHARAGANDE
NAIBU MKURUGENZI WA HABARI, UENEZI NA MAHUSIANO NA UMMA CUF-TAIFA
maharagande@gmail.com
TIGO-0715 062577
VODA-0767 062577

CHAMA CHA Wananchi CUF kimesikitishwa kwa kudai kuwa kitendo cha Jeshi la Polisi kuwateka viongozi wa chama hicho takribani 20 mkoani Pwani.



Naibu Katibu Mkuu Uenezi Jumuiya ya Vijana Chama cha Wananchi CUF Mohamed Mahmoud Mahinda amedai hayo leo kupitia ukurasa wake wa kijamii wa Facebook kuwa viongozi wa CUF katika maeneo ya Kibiti, Ikiwiri na Rufiji wametekwa na jeshi hilo na kupelekwa mahala pasipo julikana.

Kibiti, ikwiriri na rufiji itazamwe kwa jicho pana na la huruma!! #jeshi la polisi linawateka na kuwatesa viongozi wa cuf kwa faida ya nani??” Amehoji.
Kiongozi huyo amesema kuwa chama hicho kimekuwa mstari wa mbele kuhimiza, kuhamasisha na kulinda amani ya nchi, na kuiunga serikali vitendo vya kihalifu vya aina yoyote ile ni haramu katika chama cha cuf.
“Tunaposema jeshi la polisi na vyombo vyengine vya dola, vitumie uweledi katika kuwasaka na kuwakamata "wahalifu" tuna maanisha yoyote alie mhalifu achukuliwe hatua za kisheria kama zinavyopaswa kuchukuliwa bila ya kujali itikadi wala muelekeo wa KISIASA, DINI WALA KABILA, Maana UOVU hauna kabila, Dini wala itikadi ya kisiasa” Amefafanua.

Hali kadhalika amesema kitendo hicho cha Jeshi la Polisi kimewasikitisha juu ya yanayoendelea kufanywa Kibiti dhidi ya viongozi wa CUF kwani vimeanza kutoa ishara mbaya na kuonesha kuwa Jeshi la Polisi, kukosa uwezo wa kutosha katika kuwabaini waovu.

“ Jeshi la polii na vyombo vya dola wamekubali kuweka pembeni taaluma zao na kukubali kutumika kwa kuwaridhisha viongozi wa chama tawala. nasema haya nikimaanisha kwamba, haiyumkiniki uwateke viongozi wa cuf zaidi ya 20, uwapeleke kusikojulikana, (kinyume na sheria) uwatese "kinyama" uwadhalilishe utu wao kisha uwaachie warudi makwao wakiwa wahoi bin taaban!! kutokana na mateso walioyapata kutoka kwenye vyombo vinavyotegemewa kusimamia sheria za nchi yetu, kulinda raia na mali zao (bila ya ubaguzi wa aina yoyote). ni aibu na fedheha kubwa, unapoona jeshi la polisi na vyombo vya dola, vinawaaminisha raia kuwa vinapambana na uhalifu, huku wao wakiongoza, au wakifanya zaidi ya uhalifu (MATESO YA KINYAMA) dhidi ya Raia wasio na "HATIA"” Amebainisha Mahinda.
Kwa upande wa Kamanda mkuu wa Mkoa wa Pwani mara alipopigiwa simu leo na muandishi wa habari hizi majira ya saa kumi na moja jioni amesema hayupo tayari kuongelea suala hilo na hana taarifa kwani uongozi wa Jeshi la Polisi haujampa taarifa yoyote.

Kamanda huyo aliyeonekana hayupo tayari kuzungumza lolote, na kusema anafuatilia tuuhuma hizo licha ya kudai kuwa waandishi wengi wa habari leo wamempigia kutaka kujua ukweli wa tuhuma hizo.

HABARI ZILIZOJIRI LEO


Topics :
 
Support : ZENJIBARZA
Copyright © 2011. ACT WAZALENDO DIASPORA NETWORK - All Rights Reserved